Header Ads Widget

WANANCHI WANAOKABIDHIWA HATIMILIKI ZA ARDHI WATAKIWA KUZINGATIA MASHARTI




 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka wananchi wanaokabidhiwa hati milki za ardhi kuhakikisha wanazingatia masharti yaliyopo kwenye hati sambamba na kufuata mipango kabambe ya maeneo husika.


Dkt Mabula amesema hayo tarehe 17 April 2023 katika eneo la Shibula wilayani ilemela mkoani Mwanza wakati wa zoezi la kutoa Hati Milki za Ardhi kwa wananchi wa eneo hilo. Jumla ya Hati 570 ziliandaliwa kwa ajili ya kuwapatia wananchi wa eneo hilo.


 ‘’Huwezi kupata hati leo, kesho unaenda kuomba kubadili matumzi mwisho wake miji inaonekana haina maana na haipendezi na sisi tunataka Jiji la Mwanza na Ilemela ikiwemo liwe mfano, tunapima viwanja vingi kwa ajili ya uwekezaji tuzingaite kilichopo kwenye Master Plan’’ alisema Dkt Mabula.


Amewaonya wanaopata hati milki za ardhi kutobadili matumizi na kuwaagiza watendaji wa sekta ya ardhi na uongozi wa wilaya ya Ilemela kuhakikisha hakuna kubadili matumizi na badala yake wamiliki wazingatie masharti ya hati na yale matumizi yaliyopo kwenye mpango kabambe.


Akigeukia suala la utoaji Hati Milki za Ardhi katika halmashauri ya Manispaa Ilemela, Dkt Mabula ameshangazwa na idadi ndogo ya wamiliki waliojitokeza kuchukua hati ambao ni 50 kati ya 570 walioandaliwa kuchukua hati.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI