Header Ads Widget

DC NGOMA AVIFUNDA VYAMA VYA USHIRIKA KUACHA UTEGEMEZI

 





NA HADIJA OMARY LINDI.....


Viongozi wa vyama vya ushirika wa Wilaya za Ruangwa Nachingwea na Liwale vinavyohudumiwa na chama kikuu cha ushirika ( RUNALI) wametakiwa kujiimarisha kiuchumi na kuachana na mtindo wa kutegemea wahisani kwa mikopo yenye riba kubwa hatua inayofifisha uwezo wa kuhudumia wanachama 



Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hassan Ngoma alipokuwa akifunga  mafunzo kwa viongozi wa vyama vya ushirika vya msingi  yaliyofanyika katika ghara la Runali  Wilayani Ruangwa.


 Ngoma alitumia fursa hiyo kuwasisitiza viongozi wa vyama vya msingi vya ushirika kuvifanya vyama vyao  kuwa imara kwa kuwa na miradi ya maendeleo na kuongeza wanachama kwani ushirika ni biashara .



DC Ngoma pia alisema  ni imani yake  mafunzo hayo yatawasaidia viongozi wa ushirika kufanya mabadiliko na kukuza ufanisi na kuwa chachu ya maendeleo kwani yamefundisha mambo mengi ikiwemo namna ya kuandaa bajeti,kutunza vitabu vya fedha , kumbukumbu na nyaraka.


"vyama ni tasisi lazima vikuze ufanisi kwa wanachama na kuwa na miradi ya maendeleo na kusaidia jamii yenye uhitaji"amesema Ngoma. 



Kwa upande wake Meneja mkuu wa chama kikuu cha ushirika RUNALI Jahida Hasani amesema chama kimeendesha mafunzo hayo kwa viongozi vyama vya msingi lengo kubwa ni kuwejengea uwezo, kwenye nyanja mbalimbali kama uandikaji mipango biashara utunzaji kumbukumbu uandishi wa vitabu vya fedha ili waweze kuondoa tatizo la upatikanaji wa hati chafu.




"Mafunzo haya ni mwendelezo kwani chama kinafanya zoezi kama hilo kila mwaka ili kuwajenga viongozi wake" amesema Jahida


Nae Mkaguzi  kutoka COASCO Hansi Kishiwa  aliwasisitiza viongozi hao wa vyama vya ushirika kutunza taarifa katika nyaraka ili kupunguza migogoro katika ushirika vyama vyao


" Kupitia elimu niliyoitoa ni imani yangu  itawasaidaia kwani baadhi  ya viongozi wa vyama vya ushirika imekua changamoto kuweka hali halisi ya thamani ya mali za vya ushirika katika taarifa zao  lakini pia  utunzaji wa  nyaraka za ushirika pia  imekua ni changamoto ambayo inasababisha bodi zinazochaguliwa kushindwa kujua taarifa za bodi iliyopita hivyo" alisisitiza Kishiwa


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI