Header Ads Widget

MVUA ZALETA MADHARA MAKUBWA MKIMBIZI IRINGA

 


MVUA  iliyonyesha  kwa  zaidi ya masaa manne Machi 27  mwaka  huu katika mji  Iringa imesanbabisha  madhara  makubwa ya  miundo  mbinu   eneo la Mkimbizi bima  na  baadhi ya maeneo ya  Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa  baada ya barabara  inayounganisha kata  hiyo na kata ya Mtwivila kuwa  hatarini  kukatika.

Wakizungumza na matukio Daima Tv wakazi  wa  eneo hilo  Silla Kimwanga  na  Sara  Sanga   walisema  kuwa  mvua  hizo  zilianza  juzi  usiku na kumalizika jana  asubuhi   zimepelekea  barabara  hiyo   sehemu  kubwa kukatika na maji ya  mvua .

Kimwamga alisema eneo  hilo  ambalo  barabara  inakaribia kukatika  yote ni  eneo  ambalo  awali  wakala wa  barabara  mijini na  vijijini (TARURA)  Manispaa ya  Iringa  alikuwa amejenga mtaro  wa  chini ya  ardhi  wa  kupitisha maji ( karavati)  ambalo mbali ya  kujenga karavati  hilo bado  eneo hilo  kuna karavati  ambalo  limeziba  halipitishi maji  hivyo  kuepelekea maji kupia  juu ya barabara  na  kuleta madhara makubwa  eneo   hilo .

“Kero  hii ni kubwa sana kwetu  wakazi wa  eneo hilo na barabara  hii pia inaunganisha kata ya Mtwivila na iwapo barabara  eneo  hilo  haitafanyiwa kazi  upo  uwezekano mkubwa wa  watumiaji wa barabara  hii kwa kata ya Mkimbizi na Mtwivila  kukosa mawasiliano kama  watahitaji  kutumia barabara  hii .

Huku  Sara  Sanga  akiomba  uongozi wa TARURA  Manispaa ya  Iringa  kutembelea maeneo  mbali  mbali ya  mji wa Iringa  ili kutazama changamoto  iliyotokana na mvua  hizo  kwani yawezekana  maeneo mengine madhara  ni makubwa  zaidi ya hayo .

Huku  diwani wa kata ya Mkimbizi Eliud  Mvella akithibitisha  kutokea kwa madhara  hayo na  kuwa eneo hilo linahitaji ufumbuzi wa haraka  zaidi ya  kunusuru  barabara  hiyo ambayo ni moja kati ya barabara  muhimu sana katika  kata  hiyo  hivyo  madhara  hayo ni makubwa  zaidi na kutaja  barabara nyingine  zilizokumbwa na  madhara  kuwa ni pamoja na ile ya Ugele ambayo  pia  imekatika  kutokana na mvua  hizo.


Mvella  alisema   barabara  nyingi za  TARURA  zimewekwa  wakandarasi  toka mwaka jana  ila changamoto  kubwa ni makandarasi  kuwa na kazi nyingi  za kufanya  hivyo  kupelekea  baadhi ya kazi  kuchelewa kiufanyika japo  muda wa  ukamilishaji  wa kazi  bado unawaruhusu .

MKandarasi Vitus  Mushi akizungumzia  tatizo la  wakandarasi  kuwa na kazi nyingi na kuchelewesha  baadhi ya kazi alisema suala  hilo  halina  uhalisia kwani  TARURA  na  wakandarasi  wanamikataba  ya kazi muda wa kuanza na kumaliza kazi  hivyo kinachofanyika na makandarasi  kuzingatia  muda wao  wa kazi .

 

Naibu  meya  wa Halmashauri ya  Manispaa ya Iringa  Juli  Sawani akizungumzia madhara ya  mvua  hizo alisema  sehemu  kubwa ya Manispaa ya  Iringa  imekubwa na madhara japo kwa sasa ni mapema  kujua  ukubwa wa  madhara  hayo kwani tathimini  zinafanyika  kupitia madiwani wa kata   husika .

 

Sawani  alisema kwa upande wa kata ya Mkimbizi  diwani  wake  amekuwa  mbele  sana  kufuatilia  changamoto  za  miundo  mbinu na kuzifanyia kazi   hivyo kwa  hilo la barabara  kutaka  kukatika  ofisi yake itamjulischa meneja wa TARURA  ili  kupita maeneo  yote  korofi na kuyafanyia kazi .

Meneja  wa TARURA wilaya ya  Iringa  Barnaba Jabiry akizungumza   kwa  njia ya  simu  na juu ya    madhara  ambayo  TARURA  imeyapata  kutokana na mvua  kubwa  zinazoendelea  kunyesha    alisema  kuwa  changamoto  ni kubwa  kwani mbali ya maeneo hayo zipo  baadhi ya  barabara  zimefungwa kabisa  kutokana na kukatika .

 

Hata  hivyo  alisema  wanaendelea  kutatua  changamoto  za  miundo mbinu katika maeneo  mbali mbali  ndani ya  wilaya ya  Iringa  ili  kuona wananchi  wanaendelea  kupata  huduma  kama kawaida  japo  alisema kutokana na madhara  hayo ya mvua kuna  uharibifu  mkubwa  zaidi   hiyo bajeti ya matengenezo ya  barabara  itakuwa  kubwa zaidi .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI