Makamu Mwenyekiti WA Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji, Mitaji ya Umma amesema, kamati hiyo imeridhishwa na Uwekezaji katika kiwanda cha kusafisha dhahabu kilichopo katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Umma amesema, wametembelea kiwanda cha kusafisha dhahabu kilichopo Mansipaa ya Ilemela Mkoani Mwanza na kusema kuwa mradi huo unatija hivyo wanaipongeza Wizara ya Madini kwa kufanya kazi nzuri ya kulea Shirika la Madini Tanzania ( STAMICO )
Waziri wa Madini Dkt Dotto Biteko amesema amepokea ushauri kutoka kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge,Mitaji ya Umma ya iliyoagiza ikimtaka kuhakilisha Madini yote ya dhahabu yanayochimbwa nchini yasafishwe kabla ya kutoka na kwenda nje ya nchi.
KIWANDA hicho ambacho kimegharimu zaidi ya shilingi bilioni 16 ambacho kina ubia na Serikali ambayo inamiliki hisa ya asilimia 20
0 Comments