Header Ads Widget

IRUWASA KUJENGA MRADI MKUBWA UTAKAOPUNGUZA GHARAMA YA BILI ZA MAJI IRINGA NA KILOLO

 


Ujenzi wa Mradi wa usambazaji maji katika miji mitatu ndani ya mkoa wa Iringa ambao utagharimu dola milioni 105 unatarajiwa kukamilika mwaka 2027, huku ukiwa nauwezo wa kusambaza maji kwa wakazi wa Manispaa ya Iringa, Kilolo na Ilula, bila kikomo mpaka mpaka mwaka 2045.



Akiongelea mradi huo Mkuu wa wilaya ya Kilolo, Peres Magiri amewataka wananchi wa maeneo hayo kulinda chanzo hicho cha maji kutoka mto mtitu ili kuweza kufikia malengo ya pamoja ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa maeneo yaliyokusudiwa.

 

“lazima kuwe na juhudi za pamoja kwanzia kwa wadau, wananchi na serikali kwa kutoa elimu juu ya umuhimu wa mradi huo kwani umetokana na juhudi za rais Samia Suluhu Hassan ambaye ametafuta fedha hizo kutoka kwa watu wa Korea na mpaka 2027 mradi utakuwa umekamilika hivyo tunamshukuru sana”.

 

Hata hivyo, Dc Magiri amesema mradi huo utakwenda kutoa ajira kwa zaidi ya vijana 6000 ambao wote ni wazawa hivyo kuwataka vijana hao kuchangamkia fursa hizo ili kuondokana na wimbi la ukosefu wa ajira.

 


 Mhandisi Fabian Maganga, mkurugenzi wa usambazaji maji, na menejimeti ya usafi wa mazingira mamlaka ya maji Iringa (IRUWASA,) amesema wanatarajia kukusanya kiasi cha lita milioni 33 kwa siku, kutoka katika Chanzo cha maji cha mto mtitu jambo ambalo litakuwa suluhisho la upatikanaji wa maji ya uhakika na kwa gharama na fuu, kwa miji mitatu ya Kilolo kwa asilimia 85, Ilula kwa asilimia 85 na kwa manispaa ya Iringa ni asilimia 100.

 

Aidha, Mhandisi Maganga, amaongeza kuwa kukamilika kwa mradi huo, kutapunguza kilio cha wateja wa maji kutoka mamlaka ya maji Iringa juu ya ukubwa bili ambao unatokana na matumizi makubwa ya umeme katika usambazaji wa maji hayo hasa kwa wakazi wa manispaa ya Iringa.

 

“maji yatakayo toka katika mto mtitu yatasafiri takribani umbali wa kilomita 46 mpaka kufika Iringa mjini kwa njia ya mtiririko ikiwa na maana ya kwenda kupunguza gharama za kutumia umeme katika kusambaza umeme, hivyo kile kilio cha siku zote cha bili kubwa huenda kitapata suluhisho kutokana na kupata maji kwa njia ya mtiririko”.

 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI