Header Ads Widget

RAIS APONGEZWA KUHAMASISHA MAENDELEO KUINUA UCHUMI

 .               


MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM NEC) Taifa Hamoud Jumaa amempongeza Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuhamasisha maendeleo na kukuza uchumi wa nchi.


Jumaa aliaysema hayo alipowaongoza wana CCM na wananchi kuadhimisha miaka 46 ya CCM Kibaha Vijijini na kuwa Tanzania ilipofikia kwa kipindi hicho kuna mengi ya kujivunia.


Alisema kuwa wumuunge mkono Rais na kuacha maneno kwani sekta zote zikiwemo afya, elimu kujengwa, vikundi vya ujasiliamali na machinga wanawezeshwa mikopo na miradi mikubwa ya kimkakati haijasimama ikiwa ni pamoja na reli ya mwendo Kasi SGR, Bandari kavu ya Kwala, Daraja la kisasa la Wami.


Jumaa aliwataka wana CCM kuwa wamoja kuimarisha ushirikiano ili kuiletea ushindi CCM uchaguzi wa Serikali za mitaa 2024 na uchaguzi mkuu 2025 pia aliweka jiwe la msingi ujenzi wa ofisi ya kata Mtongani ambao ulianza tangu mwaka 2017 kwa njia ya kujitolea ambapo amechangia 500,000 na rafiki yake 500,000 kwa ajili ya ujenzi huo.


Naye Mwenyekiti wa CCM Kibaha Vijijini Mkali Kanusu alieleza kuwa Rais Samia apewe ushirikiano na kuyaeleza yale aliyoyatekeleza nchini na alisisitiza kwa wana CCM kuwa na umoja na mshikamano na pasipo kutengana ili chama kiweze kusonga mbele.


Katibu wa CCM Kibaha Vijijini Safina Nchimbi alieleza kuwa maadhimisho hayo yameambatana na tukio la kuchangia damu kupanda miti kufanya usafi kituo cha afya Mlandizi na zahanati


Kwa upande wake Katibu wa CCM Mtongani Gloria Kirei alisema ujenzi huo mbali ya wanaCCM kujitolea pia wabunge viti maalum Hawa Mchafu ,Subira Mgalu, wilaya na Mwenyekiti wa UWT mkoa Zainabu Vullu nao walichangia vifaa mbalimbali.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS