Header Ads Widget

DKT. BITEKO AWATUNUKU VYETI WAHITIMU 39 STASHAHADA YA TEKNOLOJIA YA MADINI YA VITO NA USONARA JIJINI ARUSHA

 



Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko amewatunuku vyeti jumla ya wahitimu 39 wakiwemo wanaume 25 na wanawake 14 wa Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) katika Stashahada ya Teknolojia ya Madini ya Vito na Usonara.


Akizungumza Dkt. Biteko katika mahafali hayo ambapo amepewa heshima ya kuongoza Mahafali ya kihistoria ya kwanza ya Stashahada ya Teknolojia ya Madini ya Vito na Usonara ya TGC amewapongeza wahitimu wote waliotunukiwa Stashahada na pongezi kwa kituo hicho kwa kuwezesha wanafunzi hao kuhitimu masomo yao.


Amesema, lengo la Serikali la kuanzisha kituo hicho lilikuwa ni kutekeleza Sera ya Madini ya Mwaka 1997 kuhusu uongezaji thamani madini nchini kwa kutoa mafunzo ya uchongaji wa vinyago vya miamba.



Ameongeza kuwa, Serikali imesisitiza kuongeza manufaa yatokanayo na Sekta ya Madini kwa kuhamasisha shughuli za uongezaji thamani madini kufanyika kwa upana zaidi hapa nchini ili watanzania wanufaike na rasilimali hiyo.


“Ili kuongeza manufaa yatokanayo na rasilimali madini nchini, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali katika shughuli za madini na kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji nchini,’’ amesema Dkt. Biteko.



Ameeleza kuwa, hatua zilizochukuliwa zimewezesha kuongezeka kwa shughuli za utafutaji madini, uchimbaji, uongezaji thamani madini, biashara za madini na kupanuka kwa biashara kutokana na shughuli za madini ha hivyo kusababisha watanzania wazawa kupata fursa za ajira na nafas iza kibiashara kupitia shughuli hizo.


Vile vile, amesisitiza kuwa uanzishwaji wa Kituo cha Jemolojia ni uwekezaji uliofanywa na Serikali katika elimu ili kuwajengea watanzania ujuzi ambao unawawezesha kuingia moja kwa moja kuajiriwa Serikalini au katika Sekta binafsi au kujiajiri.










Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS