Serikali ya Jamuhuri ya a Muungano wa Tanzania chini ya uongozi madhubuti wa Mh. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeendelea kuhakikisha kuwa; wananchi wake wanaishi kwa utaratibu maalum, mpangilio mzuri na kwa usalama zaidi kupitia maeneo wanayoishi.
Hayo yameelezwa leo na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. Ridhiwani Kikwete katika Kikao maalum cha uzinduzi wa Bodi Mpya ya Usajili ya Wataalam wa Mipango Miji kilichofanyika jijini Dodoma.
Aidha, kupitia Kikao hicho;Mh. Ridhiwani amewahimiza wataalam,viongozi na watanzania kwa ujumla kuendelea kudumisha maadili ya kazi kwa kutumia vizuri fursa ya Miradi ya ardhi inayoletwa na Serikali ili kulinda na kuendeleza Mipango Miji iliyokwisha wekwa.
0 Comments