Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo
akizungumza wakati wa Mkutano wa 10 wa Mawaziri waliopo katika Mktaba wa
Kikanda wa Usimamizi Endelevu wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika uliofanyika jijini Bujumbura nchini Burundi ambapo Tanzania ilikabidhi kijiti cha
uenyekiti kwa mwanachama Burundi baada ya kumaliza muda wa uongozi wa mwaka
mmoja.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo
akimkabidhi Waziri wa Mazingira, Kilimo na Mifugo wa Burundi Prof. Sanctus
Niragira, uenyekiti wa Mkutano wa 10 wa Mawaziri waliopo katika Mktaba wa
Kikanda wa Usimamizi Endelevu wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika uliofanyika jijini Bujumbura nchini Burundi, ambapo Tanzania imemaliza muda wake.
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Switbert Mkama akishiriki
Mkutano wa 10 wa Mawaziri waliopo katika Mktaba wa Kikanda wa Usimamizi
Endelevu wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika uliofanyika Bujumbura nchini
Burundi ambapo Tanzania ilikabidhi kijiji cha uenyekiti kwa Burundi.
Waziri
wa Mazingira, Kilimo na Mifugo wa Burundi Prof. Sanctus Niragira akizungumza
wakati wa Mkutano wa 10 wa Mawaziri waliopo katika Mktaba wa Kikanda wa
Usimamizi Endelevu wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika uliofanyika jana jijini
Bujumbura nchini Burundi, ambapo Tanzania imemaliza muda wake wa uenyekiti.
Mkurugenzi
wa Mazingira Dkt. Andrew Komba akishiriki Mkutano wa 10 wa Mawaziri waliopo
katika Mktaba wa Kikanda wa Usimamizi Endelevu wa Ukanda wa Ziwa
Tanganyika uliofanyika Bujumbura nchini Burundi ambapo Tanzania
ilikabidhi kijiji cha uenyekiti kwa Burundi.
Afisa
Mazingira Mkuu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Deogratius Nyangu akishiriki
Mkutano wa 10 wa Mawaziri waliopo katika Mktaba wa Kikanda wa Usimamizi
Endelevu wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika uliofanyika Bujumbura nchini
Burundi ambapo Tanzania ilikabidhi kijiji cha uenyekiti kwa Burundi.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo
akiwa na viongozi mbalimbali wakati wa Mkutano wa 10 wa Mawaziri waliopo katika
Mktaba wa Kikanda wa Usimamizi Endelevu wa Ukanda wa Ziwa
Tanganyika uliofanyika jijini Bujumbura nchini Burundi ambapo
Tanzania ilikabidhi kijiti cha uenyekiti kwa mwanachama Burundi baada ya
kumaliza muda wa uongozi wa mwaka mmoja.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Serikali ya Tanzania imeikabidhi Burundi kiti cha
uenyekiti wa Mawaziri waliopo katika Mkataba wa Kikanda wa Usimamizi Endelevu
wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika na kusisitiza Kiswahili kitumike kama lugha
kuu ya mawasiliano katika mikutano yote itakayofanyika.
Hayo yamefanyika wakati wa Mkutano wa 10 wa Mawaziri hao uliofanyika
jana jijini Bujumbura nchini Burundi baada ya Tanzania kumaliza muda wa
uenyekiti uliodumu kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Akizungumza wakati wa
mkutano huo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe.
Dkt. Selemani Jafo alisema Tanzania inashiriki katika shughuli zote zinazolenga
kuhakikisha usimamizi endelevu wa rasilimali za ziwa hilo.
Pia, alisema Tanzania imedhamiria kushirikiana
na nchi wanachama ambazo ni Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na
Zambia katika utekelezaji wa programu za kikanda zinazolenga kulinda rasilimali
za pamoja za Ziwa Tanganyika na kuboresha maisha ya watu katika bonde hilo.
Dkt. Jafo alisema Ziwa Tanganyika ni rasilimali muhimu kwa
wananchi takriban milioni 10 wa ukanda huo wanaolizunguka hivyo zinahitajika
juhudi za pamoja katika kulilinda.
“Waheshimiwa mawaziri, mazingira tunayoishi yanabadilika
haraka sana na shughuli za binadamu zinatumia maliasili za dunia kwa kasi ya
kutisha na kuharibu mifumo ikolojia. Inakadiriwa kuwa zaidi ya viumbe 22,000
wako hatarini kutoweka ikiwa ni pamoja na baadhi ya viumbe katika Ziwa
Tanganyika,” alisema.
Hivyo, alitoa wito kwa Mawaziri hao
kutoka nchi wanachama kuungana kwa pamoja kujadili namna bora ya kulinda Ziwa
Tanganyika kwa leo na kizazi kijacho huku akisisitiza umuhimu wa kuweka
utaratibu wa muda mrefu wa ufadhili wa programu ya maendeleo ya Ukanda ya Ziwa
Tanganyika.
Ujumbe ulioshiriki katika Mkutano huo uliwashirikisha
pia Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Switbert Makama,
Mkurugenzi wa Mazingira Dkt. Andrew Komba, Afisa Mazingira Mkuu Ofisi ya Makamu
wa Rais Dkt. Deogratius Nyangu na uwakilishi wa Wizara ya Fedha na Mipango pamoja
ba Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
0 Comments