Header Ads Widget

KAMPUNI YA MANTRA YAIMARISHA USHIRIKIANO NA WAFANYAKAZI WA HIFADHI YA NYERERE ILIYOPO KATIKA KANDA YA LIKUYUSEKAMANGA

 

Katika kuimarisha uhusiano na ujirani mwema, kampuni ya Mantra Tanzania Limited inayomiliki mradi wa madini ya Urani wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma, imekabidhi jenereta na jokofu vyenye thamani ya zaidi ya Tshs. Millioni 25 kwa wafanyakazi wa hifadhi ya Taifa ya Nyerere kanda ya Likuyusekamaganga iliyopo wilayani humo.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Mantra Tanzania Ndugu Alexander Ryabchenko amesema kuwa, tukio hili ni ishara ya ujirani mwema kwani kampuni hii haitazamii kuwa na mahusiano mazuri tu na jamii inayozunguka mradi, lakini pia na taasisi za serikali na binafsi ambazo kwa namna moja au nyingine ni wadau muhimu wa kampuni hiyo na wilaya nzima ya Namtumbo.

Vilevile ndugu Beria Voster ambaye ni Msimamizi wa Mradi huo wa urani, ametoa shukrani za dhati kwa wahifadhi kwani wamekuwa wakionesha ushirikiano wa pekee kwa kampuni ya Mantra Tanzania na kuhimiza kudumisha ushirikiano huu baina ya taasisi hizo mbili kwani wote wana nia njema ya kujenga na kuchangia ukuaji wa uchumi katika taifa letu.

“Huu si mwisho bali ni mwanzo mzuri wa ushirikiano wetu endelevu, tukio hili ni ishara ya shukrani kutoka kwa kampuni ya Mantra kwani mara zote TANAPA kupitia hifadhi hii ya Nyerere imekuwa msaada mkubwa katika nyanja mbalimbali ikiwemo ulinzi dhidi ya wanyama wakati shughuli za mradi zinapoelekea katika hatua za mwanzo za uchimbaji” Alisema Ndugu Voster.

Nae Ndugu Shangwe Kakulu kwa niamba ya wafanyakazi wenzake wa TANAPA waliopo katika hifadhi ya Nyerere kanda ya Likuyusekamaganga ametoa shukrani za dhati na kusisitiza kuwa ushirikiano huo baina yao na kampuni ya Mantra utazidi kuwa endelevu kwani mbali na majukumu ya kazi, taasisi hizo zimekuwa marafiki wazuri pamoja na taasisi zingine ambazo ni wadau wa TANAPA. Bwana Kakulu alisisitiza kuwa, ushirikiano huo utaendelezwa baina ya pande zote mbili ili jamii izidi kunufaika kutokana na uwepo wa taasisi hiyo ya uhifadhi na mradi huo wa Mantra.

Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Mantra Tanzania Bi. Khadija Kawawa amesema kuwa mbali na kufanya majukumu ya kijamii ambayo Mantra hujihusisha nayo mara kwa mara, kampuni ya Mantra inatazamia kuendeleza ushirikiano kwa wadau wake wa karibu na muhimu kama ilivyofanya kwa wafanyakazi hao wa hifadhi ya Nyerere wa kanda ya Likuyusekamaganga. “Hii ni ishara sio ushirikiano tu, bali upendo ambao kampuni ya Mantra inao kwa wadau wote wa maendeleo waliopo wilayani Namtumbo na Ruvuma kwa ujumla.

Kwa upande wa watumishi hao wa hifadhi ya Nyerere kanda ya Likuyusekamaganga wameishukuru kampuni ya Mantra kwa kuwa ushirikiano na kuahidi kuudumisha huku ikiendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kuhudumia na kulinda hifadhi hiyo ya taifa.

Ndugu Shangwe Kakulu akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wa hifadhi ya Nyerere kanza ya Likuyusekamaganga katika kupokea jokofu na jenereta kama ishara ya ushirikiano baina ya wahifadhi hao na Mantra Tanzania

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mantra, Alexander Ryabchenko akizungumza wakati wa makabidhiano ya jenereta na jokofu kwa wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere kanda ya Likuyusekamaganga.

Ndugu Shangwe Kalulu akionesha uongozi wa Mantra eneo ambalo watahifadhi jenereta lililokabidhiwa na kampuni ya Mantra Tanzania Limited

Mkurugenzi Mtendaji wa Mantra akioneshwa eneo ambapo jokofu litapowekwa na kuhudumia wafanyakazi wa hifadhi

Msimamizi wa Mradi wa Mantra Tanzania Limited Ndugu Beria Voster akizungumza kutoa shukrani kwa wafanyakazi wa hifadhi ya Nyerere kwa ushirikiano wana zidi kuuonyesha kadri mradi unavyoendelea



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS