Header Ads Widget

WATATU WAUAWA NA JESHI LA POLISI KAGERA

 



NA TITUS MWOMBEKI, Matukio Daima App.


JESHI la Polisi Mkoani Kagera limefanikiwa  kuwaua  watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi katika mipaka ya  wilaya ya Ngara na Biharamulo mkoani Kagera.


Hayo yamesemwa na kamanda wa Jeshi la  Polisi mkoa wa kagera,  ACP William Mwampagale wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema kuwa jeshi hilo lilifanya operashani maalumu baada ya kupata  taarifa  kuwa kuna kundi lililokuwa linapanga  kufanya uhalifu.


" Jeshi la polisi mkoani kagera  lilifanya operasheni na msako  mnamo Novemba 15 mwaka huu kufuatia taarifa za kiintelijensia kuwa kuna kikundi cha majambazi kimepanga kufanya uhalifu kwa kutumia silaha na mnamo mwezi Novemba 15, 2022 tuliweza kuweka mitego katika maeneo  hayo ambapo   watatu wenye jinsia ya kiume wanaosadikiwa kuwa majambazi kujeruhiwa kwa risasi wakati wa majibizano ya risasi kati yao na 

Jeshi la polisi  hivyo wakati wanakimbizwa  hospitali walipoteza maisha na miili yao imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Ngara Nyamiaga" 


Amesema  majambazi hao walikuwa watano jinsia ya kiume waliokuwa wanakadiliwa kuwa na umri wa miaka 25-35 na  katika uchunguzi wa awali uliofanya na jeshi hilo umebaini kuwa kikundi cha watu hao kimekuwa kikifanya matukio ya unyang'anyi wa kutumia silaha tangu mwezi Septemba na Oktoba mwaka huu katika maeneo ya kijiji cha Bugarama,Muganza na Murusagamba.


Hata hivyo Mwampagale ameongeza kwa katika operashani hiyo wamefanikiwa kupata silaha moja aina ya AK47 isiyokuwa na namba pamoja na magazine moja ikiwa na risasi 12 na hivyo kutumia nafasi hiyo kuwaonya wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo.


Sambamba na hilo jeshi la polisi mkoa wa Kagera amewataka wananchi wa mkoani humo kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa sahihi za uhalifu pamoja na wahalifu ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao kabla ya madhara kutokea.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI