Header Ads Widget

VIJANA WAMESHAURIWA KUJIUNGA NA VYUO VYA UFUNDI STADI ILI KUPATA MAFUNZO YA VITENDO AMBAYO YATAWAWEZESHA KUJIAJIRI.

 

WITO umetolewa Kwa vijana kujiunga na vyuo vya Ufundi Stadi ili kuwa na ujuzi utakaowawezesha kujiajiri wenyewe Katika sekta binafsi .


Wito huo umetolewa jana na mkurugenzi wa Kampuni ya( CF) Chesco Ng’umbi ambaye alikuwa ni mgeni rasmi katika mahafali ya saba katika chuo cha ufundi stadi R.D.O Mdabulo, Mufindi na kuelezea kuwa vijana wengi wanapohitimu masomo yao wanajikuta kuwa tegemezi kutokana na kutegemea kupata ajira jambo ambalo kwa sasa limekuwa ni gumu.

 


Chesco amesema mafunzo ambayo wanafunzi wanayapata katika vyuo vya R.D.O hapa nchini yanawezesha vijana kupata ajira kwa wakati au kujiari wenyewe kutokana na uzoefu ambao hautegemei vyeti pakee.

 

Naye mkurugenzi wa Rural Development Organization (RDO) Fidelis Filipatali amesema chuo hicho kinajivunia mafanikio mbali mbali kwa jamii inayowazunguka tangu kuanzishwa kwake miaka 20 iliyopita, kwani kimetoa misaada mbali mbali Pamoja kuwalipia ada ya masomo wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu.

 

Aidha Fidelis amekumbusha wahitimu hao Kwenda kufanya kazi kwa vitendo kama ambavyo wamefundishwa chuoni hapo ili kuweza kupata ajira kwa wakati au kujiajiri wenyewe.

 

Nao baadhi ya wanafunzi waliohitimu mafunzo hayo wamekishukuru chuo cha ufundi stadi (RDO) kwa msaada wa mafunzo waliyowapatia kwani wamefanikiwa kujifunza kwa vitendo mafunzo mbali mbali ambayo yatawawezesha kukabiliana na changamoto ya ajira inayoikabili dunia kwa sasa.














Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI