Header Ads Widget

RC MGUMBA AAGIZW WATUMISHI 24 WAKAMATWE TANGA

 


NA AMINA SAID,MATUKIO DAIMAAPP

TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga Omary Mgumba ameiagiza kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa  wa Tanga kuwakamata  huku  wakisimamishwa kazi ,watuhumiwa wapatao 24 waliojihusisha na kuungua kwa  ghala la kuhifadhia mizigo ya TRA katika bandari ya Tanga,ili kufikishwa kwenye vyombo vya sheria  kujibu tuhuma zinazowakabili.


Mkuu wa mkoa wa Tanga alitoa agizo hilo  baada ya kupokea taarifa ya  kamati maalumu ya kuchunguza kutokea kwa Moto  katika ghala hilo kuanzia tarehe 29 November mwaka huu. 


Aidha Mkuu wa mkoa wa  Tanga  aliunda kamati hiyo ya uchunguzi mara baada ya kutokea kwa tukio la   kuungua moto  ghala lenye  vitu mbalimbali  ambavyo bado havijalipiwa ushuru liliotokea majira  ya saa nane na nusu usiku  mnamo tarehe 23  October mwaka huu. 

 

Mgumba liwataja badhi ya watuhumiwa ambao wanatakiwa kusimamishwa kazi  ili kupisha uchunguzi ambao ni watumisha sita wa mamalaka ya bandari Tanga ambao ni  Bw.Fortunas Sandaria mlinzi wa mwandamizi,Bwa.Aliko Mwakipangala, Bwa.PeterMwankana ,Issa  Haruna  Abdalah ,James Kyaomoka ,Susan Kanyika mlinzi mwandamizi .


Aidha  alisema watumishi wengine ni watumishi saba wa SUMA JKT, Watumishi wa saba wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA  ,mtumishi wa moja wa TBS  ambaye ni mkaguzi wa TBS Tanga wengine ni raia kwaida 3 ambao ni wamehusika kula njama na kuisababishia serikali hasara.


 Sambamba  na hayo aliwataka  mameneja wa Bandari mkoa Wa Tanga na TRA mkoa wa Tanga kutokana  na uzembe huo wa taarifa kutofautiana walinzi kupangwa wale wale  wajitathimini na kuwajibika.


Aidha aliwaomba Kamishna wa TRA  na Mkurugenzi mtendaji wa Bandari Tanzania kuwachukulia hatua watumishi ambao wamegundulika na makosa ya kiutendaji waweze kuwajibishwa.


Awali akisoma taarifa ya uchunguzi wa tukioa la kuungua kwa ghala ya bidhaa na mizigo mbalimbali  ya TRA katika Bandari ya Tanga Mwenyekiti wa kamati  maalumu  Sebastian  Masanja  alisema kamati iligindua kulikuwa na uwepo wa mkaa nyuma ya ghala  ambayo sio kawaida kuwepo kwani hakuna shughuli zygote za mama ntilie iliyowahi kufanyika hapo.


Samabamba na hayo alisema kuwa taarifa ya zilitofautia na kati ya meneja wa TRA na Bandari  kwani wanatoa mizigo kwa gets namba moja  badala ya geti namba mbili ambapo geti hilo ni la Abiria. 


Aidha kamati hiyo ilishauri kwamba Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa  TAKUKURU  jeshi la Polisi waendelee na uchunguzi ili wahusika kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI