Header Ads Widget

WANANCHI NJOMBE WALALAMIKIA UBOVU WA MIUNDOMBINU


Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE                                                                                                                                                            

Wananchi wa kijiji cha Igombola kata ya Lupembe Wilaya ya Njombe  wamelalamikia  ubovu wa miundombinu  ya barabara ya kwenda Zahanati pamoja na maeneo ya vijiji vingine vya kata ya mfiriga kwani imekuwa ikiwakwamisha kiuchumi na kuhatarisha maisha yao.


Katika mkutano wa hadhara wa mkuu wa Wilaya ya Njombe baadhi ya wakazi hao akiwemo Peter Kyamani na Lucy Mligo Wamesema ubovu wa barabara hasa wakati wa masika umekuwa ukikatisha mawasiliano pamoja na mazao kuozea shambani.


Awali diwani wa kata ya Lupembe Michael Mbanga amesema changamoto ya miundombinu ya barabara ni kubwa hususani katika kipindi cha masika kwani shughuli za kiuchumi zimekuwa zikisimama.


Mtaalam wa ujenzi toka Wakala wa barabara za mijini na vijjini TARURA wilaya ya Njombe Mhandisi Mussa Mwansule amekiri kuwapo kwa changamoto ya miundombinu hiyo huku akisema itatazamwa katika bajeti ya mwaka ujao kwani kwa sasa hakuna bajeti.


Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Njombe Kissa Kasongwa amesema ni muhimu TARURA wakaona namna ya kwenda kufanya marekebisho hata kwenye maeneo korofi badala ya kuacha kabisa  barabara kusubiri mwaka wa fedha ujao huku akiwataka watumishi kuwasikiliza madiwani wanapowafuata kuwaeleza kero mbalimbali.


Mkuu wa wilaya ya Njombe katika ziara yake  ametembelea na kufanya mikutano katika kijiji cha Igombola kata ya Lupembe pamoja na vijiji vya  Madeke na  Mfiriga kata ya Mfiriga.






Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI