Header Ads Widget

TASWIRA YA KIWANJA CHA NDEGE CHA KIMATAIFA CHA MSALATO MKOANI DODOMA

 















Taswira ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato Mkoani Dodoma itakavyoonekana mara baada ya kukamilika kwa Ujenzi wake ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameweka jiwe la Msingi la mradi huo Mkubwa nchini.

 

Katika Awamu ya kwanza, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato utakuwa na uwezo wa kuhudumia Ndege kubwa aina ya Dreamliner 787 yenye uwezo wa kubeba abiria 350. Aidha, uwanja huo utakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni 1.5 kwa mwaka na utakuwa na miundo mbinu mbalimbali kama mnara wa kuongozea Ndege, Jengo la Watu Mashuhuri, jengo la Zimamoto, mizigo, Jengo la Rais, pamoja na Karakana.

 

Mradi wa Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Msalato Mkoani Dodoma unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2024.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI