Header Ads Widget

TANESCO TABORA INATHAMINI MCHANGO WA TAASISI NA WATU BINAFSI .

 


Na Lucas Raphael,Tabora

Shirika la umeme mkoa waTabora Tanesco limetoa zawadi ya ngao kwa  Taasisi na watu binafsi walifanya vizuri  kwa kulipa bila za umeme baada ya kupata huduma hiyo kwa mwaka huu kwa lengo la kutambua mchango wao kwa shirika   .

Akizngumza katika hafla fupi ya kuwapongeza wateja hao meneja wa shirika hilo mkoa wa Tabora mhandisi Khadija Mbarouk iliyofanyika katika ofisi za shirika hilo jana

Alisema kwamba shirika limechukua hatua hiyo ya kuwatambua wateja hao wa kubwa ,baada ya kuonyesha jitiada za kuchangia pato la shirika na serikali kwa ujumla .

Alisema kwamba licha ya shirika kutoa huduma pia linafanya biashara ya usambaza uememe kwa wateja wake hivyo wanawajibu wa kulipa bili zao kila mwezi na kila mwaka kwa wakati.

Mhandisi Khadija alisema kwamba katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja tumeona kutambua wateja wachache waliweza kutumia huduma ya Tanesco na kulipa zaidi ya shilingi milioani 200  kwa mwaka

Meneja huyo wa Tanesco mkoa wa Tabora aliwataja wateja huo kuwa ni  Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira mkoa wa Tabora (TUWASA) iliyotumia huduma ya umeme na kulipia kiasi cha shilling milioni 764,831,278 kwa mwaka huu .

Alisema kwamba licha ya Tuwasa pia Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira wilaya ya Nzega( NZUWASA) ambayo ilitumia huduma ya  hiyo na kulipia kiasi cha shilingi milionbi 164,898,690 kwa mwaka huu.

Wengine ni Kampuni ya simu za mikono ya TTCL ambayo imelipa kiasi cha shilingi milioni 51,083,142 kwa mwaka  na Kampuni ya uchenjuaji wa Dhahabu wilayani Igunga mkoani hapa ya Taur Tanzania ilifanikiwa kulipa kiasi cha shilingi milini 217,976,835 kwa mwaka huu.

Alimtaja mteja mwingine ni  mmiliki wa Hotel ya JM, Jimmy Marco aliyelipa kiasi cha shilingi milioni 25,705,592 mwaka  huu  .

Akizungumza kwa niaba ya wateja wengine mwakilishi wa mkurungezi wa Mamlaaka ya maji safi na usafi wa mazingira mkoani Tabora Tuwasa Namyaki Moleli alisema kwamba wanalishukuru shirika la Tanesco kwa kufanya kitu kama hiki amchao kinachochea ujirani mwema licha ya kupita bilia kwa wakati

Alisema ni wajibu kwa kila Taasisis na watu binafsi wanatumiahuduma ya  umeme au huduma yoyote nyingine ikiwemo maji kukumbuka kulipa bila kwa wakati .

“ umeshapata huduma na umetumia huduma ndivyo hivyo hivyo inakupasa kukumbuka kulipa bili kila mwezi ulipotumia huduma hiyo .alisem Namyaki  


Wiki  ya huduma kwa mteja inaadhimishwa kila mwaka kuanzia wiki ya kwanza ya mwezi octoba .

NI mwakilishi wa mkurungezi wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira TUWASA Namyaki Molel akiwa katika picha ya pamoja  meneja wa shirika hilo mkoa wa Tabora mhandisi Khadija Mbarouk aliyevaa hijab  na katikatika ni  mkurungezi wa Tanesco kanda ya magharibi Mhandisi Richard Swai.

 

NI Mkurungezi wa Tanesco kanda ya Magharibi Mhandisi Richard Swai ,akiwa amesimama ni Meneja wa shirika hilo mkoa wa Tabora mhandisi Khadija Mbarouk wakiwatazama watumishi wa shirika hilo baada ya kufurahia jambo katika Hafla fupi

 


NI Mkurungezi wa Tanesco kanda ya Magharibi Mhandisi Richard Swai akimkabidhi  ngao ya shindi kwa kwanza kwa walipaji wa kubwa wa bili za umeme mkoani Tabora mwakilishi wa mkurungezi wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira TUWASA Namyaki Molel na aliyevaa hijab ni Meneja wa shirika hilo mkoa wa Tabora mhandisi Khadija Mbarouk.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI