Header Ads Widget

SERIKALI YAOMBWA KUTHAMINI SHULE ZA WATU BINAFSI NCHINI



 Ilemela English Medium Primary School iliyopo Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza imefanya mahafali ya (5) ya darasa la saba katika shule hiyo ambapo wamehitimu wanafunzi 30, wavulana 16 na wasichana 17 ambao walianza darasa la kwanza mwaka 2016 wakiwa wanafunzi 33.



Mkurugenzi wa Ilemela English Medium Primary School David Maduhu ameiomba Wizara ya Elimu  kuthamini shule za binafsi kama inavyothamini shule za serikali kutokana na kuzichukulia kama za upinzani huku ukizingatia shule hizo zimekuwa zikiongoza katika matokeo ya mitahani yoyote 



Mwalimu mkuu wa Ilemela English Medium Primary School Sande Jackson wazazi wanaosomesha watoto katika shule hiyo kutoa ushirikiano wa kushiriki makambi ya masomo katika shule hiyo ili kuwaongezea ufanisi wa kufanya vizuri katika masomo pamoja na mitihani.


Ilemela English Medium Primary School imepanda kitaaluma mwaka jana na kupata alama A katika matokeo ya mtihani wa Taifa na katika mitihani ya Kata ,wilaya na mkoa imeshika nafasi ya 3 na kupata wastani wa A kwa mitihani yote na mwaka huu wanatarajia kushika nafasi ya 10 bora kitaifa.








Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI