Header Ads Widget

Mwenyekiti UVCCM KIBITI ASHINDA KWA KISHINDO UENYEKITI CCM WILAYA

 


Na Scolastica Msewa,KIBITI

KIJANA Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Kibiti alipindua meza  kwa kupata ushindi wa kishindo kwa kutwaa nafasi ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Kibiti Mkoani Pwani Juma Kassim Ndaruke ambaye ameibuka kidedea kwa kupata kura 428 huku Mwenyekiti  aliyekua aliyemaliza muda wake  Abdullatif Jabir Malombwa aliyepata kura 385.


Uchaguzi huo ambao ulionekana kuwa na ushindani wa hali ya juu huku uongozi uliomaliza muda wake ukionekana kuwa  na wafuasi kadhalika kwa yoande wa kundi la vijana wakionyesha kuwa na kiu ya kunyakua taji hilo ikiwa ni katika lengo lakundeleza gurudumu la maendeleo  Wilayani Kibiti.


Awali ya yote uchaguzi huo ulianza ukiwa katika ulinzi wa hali ya juu ambapo vyombo vya usalama wakionekana kuimarisha ulinzi pamoja na TAKUKURU wakiwepo eneo.la tukio na kuonekana kusimama imara.


Aidha uchaguzi huo ulisimamiwa na  Katibu wa Jumuia ya Wanawake  Mkoa wa Pwani Fatma Juma Ndee ambapo kabla ya kuanza kwa uchaguzi alitangaza zoezi la kuwahakiki wajumbe wote kutoka katika kata 16  za Kibiti ambapo pia waliweza kuwabaini baadhi ya wapigakura ambao waliku wajumbe feki na kuamuru vyombo vya usalama  kuwatoa nje na baada ya hapo zoezi liliendelea.


Wengine walioshiriki kwenye kinyang'anyiro hicho ni  Mwenyekiti  aliyekua aliyemaliza muda wake  Abdullatif Jabir Malombwa aliyepata kura 385 huku akifuatiwa na  Abdallah Seif Mpili aliyeambulia kura 7.


Aidha Wajumbe waliochaguliwa  katika mkutano huo  wajumbe wa mkutano mkuu Taifa CCM  ni Ally Seif  Ungando  ,Khalid Mtarazaki na Rehema Jumanne Mkumba.


Wajumbe  wengine wa mkutano mkuu CCM Mkoa ni Ashura  Matimbwa na Uwesu Mtandika.


Baada matokeo kutangazwa Halmashauri Kuu CCM  Wilaya ilikaa kikao na kumchagua Katibu Mwenezi wa Siasa na Itikadi ambaye aliyeshinda ni Juakali   kuwa ndiye  Katibu Mwenezi CCM Wilaya  ya Kibiti.


Mbunge wa Jimbo la Kibiti Mheshimiwa Twaha Mpembenwe alisema amesuuhudia uchaguzi huo kuwa ulikuwa wa haki na umezingatia kanuni na katiba ya Chama cha Mapinduzi hata kuweza kuwapata viongozi waliopata nafasi walizoomba akiwemo Mwenyekiti wa CCM Wilaya hiyo.


Alisema ameahidi kuwapa ushirikiano na kwamba hanashaka  na maamuzi ya WANACCM waliyofanya kumchagua Mwenyekiti wa CCM waliomchagua hasa kwa uzoefu aliokuwanao wa kuongoza jumuhiya ya Vijana wa CCM katika miaka mitano iliyopita.








Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI