Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mheshimiwa Queen Sendiga ametoa maagizo kwa wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha wanashirikiana na wataalamu kutafuta ufumbuzi utakaowezesha miradi ya maendeleo kukamilika kwa wakati.
Mkuu huyo wa Mkoa ametoa maagizo hayo leo Jumatano (24.08.2022) mjini Sumbawanga alipoongoza kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa maagizo mbalimbali ya serikali kilichohudhuriwa na Wakuu wa Wilaya za Sumbawanga, Nkasi na Kalambo, Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala Wilaya, Wakuu wa Idara, Seksheni na Vitengo
0 Comments