Header Ads Widget

MAKAMU WA KWANZA NA WA PILI WA RAIS ZANZIBAR WAJIANDIKISHA KWENYE MBIO ZA TIGO ZANTEL ZANZIBAR INTERNATIONAL MARATHON

 

 



MAKAMO wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mh. Othman Masoud Othman amekuwa miongoni mwa viongozi wa juu waliosajiliwa kwa ajili ya Ushiriki wa mbio za Kimataifa za Zanzibar zinazofahamika Tigo Zantel International Marathon,


Mh.Masoud amesajiliwa  na Kamati ya mbio hizo, mapema leo ofisini kwake migombani,Visiwani Zanzibar.


Aidha, Kamati hiyo pia imeweza kumsajili Makamo wa Pili wa Rais, Mh.Hemed Suleiman Abdullah, 



Pia imewasajili Kamishna wa Police Zanzibar (CP) Hamad Khamis Hamad, Ofisini kwake na Kamanda wa KMKM.


Kamati hiyo, pamoja na mambo mengine iliweza kuwajulisha viongozi hao, kuhusu matukio yote yatakayofanyika siku ya Tarehe 5 na 6 katika ufukwe wa Mercury (Mizingani Road) na pia siku ya Marathon tarehe 7, itakayoanza  kuanzia saa 12 za asubuhi.


Kamati hiyo pia anaendelea na usajili kwa viongozi na wengineo huku pia zoezi la kujisajili likiendelea katika vituo mbali mbali vilivyopo Dar es Salaam katika maduka ya 

Just Fit Mlimani City na Kijitonyama kwa waliopo Dar es salam  na walio Zanzibar  zoezi la usajili linaendelea katika jengo la Michenzani Mall, Mgahawa wa Mercy na Catalunia- Kiembe samaki au kwa njia ya kielectroniki kupitia App ya (Nilipe) au kwa Lipa namba 5121222  kutoka kwenye mtandao wako wowote." Ilieleza taarifa hiyo ya Kamati ya mbio.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI