Header Ads Widget

KAMISHNA WA ADC AIRINGA AMWANDIKIA BARUA RAIS SAMIA


 WAKATI Rais Samia Sulua Hassan anataraji  kuanza ziara  yake   Agosti 11 mwaka huu katika mkoa wa  Iringa,kamishna  wa  Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC ) mkoa  wa  Iringa  Daud Masasi amesema amemwandikia  Rais  barua ya  wazi  yenye  mambo makuu matano kama  sehemu ya kutambua jitihada  za  serikali ya  awamu ya  sita na  kumshauri kufanyia kazi mambo  hayo aliyoandika kwenye barua  hiyo.

Akizungumza  na  wanahabari leo  mjini  Iringa Masasi  alisema  kuwa  barua  hiyo  aliiandika toka  Mei 16 mwaka  huu  na kuwa  jambo la kwanza alilimwandikia  Rais Samia kwenye  barua ni hiyo ni juu ya Lugha adhimu ya  Taifa Kiswahili   kuhakikisha  chati ya  kuwa miongoni mwa  lugha  kuu ya dunia kwa  kuona  kiswahili  kinatendewa  haki  na  hatua  zinachukuliwa kulinda,kuendeleza  lugha  hiyo.
 
Masasi  ametaja  jambo la  pili katika  barua hiyo ni suala la utamaduni na  michezo  kuwa  utamaduni   mambo  hayo ni msingi sana katika  Taifa  kwa maana ya  Lugha ,mavazi , chakula ,ngoma za makabila ,mila na destuli na mengine na  msingi  bora wa Taifa  ,jambo la tatu ni ardhi  na kilimo wakati  jambo la Nne katika barua hiyo ni majina ya  mikoa na mwisho  ni  kuufanya  mkoa  wa  Iringa  kuwa na hadhi ya muonekano  wa  jiji.

" kama  miji  mingi nchini  imekuwa  kwa kasi  na idadi ya watu inaongezeka sana  katika  mji  wa Iringa  panaitwa  Miyomboni  enzi hizo  kulikuwa na miti  hiyo aina ya miyombo  wakati  kata ya Kitanzini  jina la makumbusho ya  kitanzi  kilichotumika kunyongea watu kipindi  cha wakoloni na  ndioa  eneo  lenye maduka na shughuli  nyingi za kila  siku" alisema 

Kuwa  wafanyabiashara wenye   maduka  asilimia 99 wana  vyombo  vya usafiri  lakini  watu  wengine  wanalazimika kufika katikati ya  mji  huo wa Iringa  kwa usafiri  ila wanakosa maeneo ya kuegesha magari yao  na kama  mji  utapewa  hadhi ya jiji  ni wazi maeneo ya maegesho  yataboreshwa  zaidi.

Pia  alisema kwa  sasa  ni wakati muafaka  wa  soko kuu la Iringa ambalo  ni la miaka  mingi  sana  kuboreshwa maana  soko hilo ni la  enzi  za mkoloni miaka ya 1960 hivyo  limechoka .

Masasi  alisema jambo  kubwa  zaidi ni  kuufanya mji wa Iringa  kuwa na  sura ya kivutio  kwa  kuona mji  huo  unajengwa  kisasa  zaidi  ili  kuendelea  kubaki kuwa lango la utalii wa  nyanda  za  juu kusini  na  kuhakikisha eneo la Gereza la  Iringa mjini linahamishwa  kwenda  nje ya  mji  huo eneo la Mlolo.

" Mheshimiwa Rais  Samia , Iringa City  inafaa kujengwa  eneo hilo la gereza  la Iringa  ambalo kwa  sasa  lipo mjini kabisa   na ndugu  zetu wa  gereza  wanaweza  kuhamishiwa  maeneo mengine  mengi yaliyopo  nje ya mji  na  huko  kupata nafasi  nzuri na kubwa ya  kujenga  gereza  na kufanya  shughuli  za  uzalishaji  tofauti na  sasa "

Hata   hivyo Masasi  amepongeza  jitihada  kubwa  za  kiubunifu  zinazofanywa na Rais  Samia katika  kutangaza utalii  kupitia The  Royal  Tour  kuwa  ni ubunifu  mkubwa  wenye   tija  kwa sekta ya  utalii na  uchumi wa  nchini .

Wakati huo  huo Masasi amepongeza  upanuzi wa  uwanja  wa Ndege  Iringa (Nduli)  kuwa  utachangia kwa  kiasi kikubwa  kukuwa  wa setika ya  utalii katika  mkoa wa Iringa kwa  kuongeza idadi ya  watalii  wanaotembelea  hifadhi ya taifa ya  Ruaha.

Pia kuhusua  suala la ruzuku ya Mbolea  ambalo  Rais Samia  ametangaza  kuanza mapema mwezi huu  alisema  ni jambo kubwa ambalo  litaongeza kasi ya uzalishaji kwa  wakulima wa mkoa wa Iringa na Taifa .


Katika hatua  nyingine Masasi  aliwataka  watanzania  kuepuka  kushawishika na  baadhi ya  wanasiasa  wasio na nia  nzuri kwa Taifa  ambao  wanataka  kupotosha  juu ya zoezi la  sensa ya watu na makazi na  kuwa  suala la  sensa ya  watu na makazi ni la taifa na kila mmoja anapaswa  kushiriki katika  zoezi hilo Agosti 23 mwaka  huu.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI