Header Ads Widget

WAZIRI MKUU AWAONGOZA WANANCHI WA RUANGWA KUTAZAMA THE ROYAL TOUR

 



Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa  leo Julai 08, 2022 ameongoza umati mkubwa wa wananchi wa wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi  kutazama Filamu ya The Royal Tour kwenye uwanja wa  Wandorwa wilayani hapa.


Akizungumza katika tukio hilo, Mheshimiwa Majaliwa ameutaka uongozi wa wilaya hiyo kuibua vivutio vya utalii ili wilaya  iweze kunufaika na idadi kubwa ya watalii wanaoingia nchini na hasa baada ya hamasa kubwa iliyochochewa na filamu ya The Royal Tour.



“Migodi ya madini mbalimbali inayotarajiwa kufunguliwa hapa hivi karibuni ni fursa ambayo wakazi wa Ruangwa mnapaswa kuichangamkia kwa kuwekeza katika miundombinu itakayowawezesha wageni watakaokuja kupata huduma muhimu ikiwemo malazi, chakula, usafiri  na huduma za afya ili kujipatia fedha”




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI