Header Ads Widget

VIONGOZI BUTIMBA MWANZA LAWAMANI

 


Mtendaj wa kata ya Butimba jijini Mwanza  bw David Kyarwenda pamoja na mwenyekiti mtaa wa Mahina  bi Mery Sule washutumiwa kuongoza wa vurugu za mgogoro wa ardhi katika eneo la kambarage, baina ya wananchi na mfanyabiashara maarufu Alhaj Yusuph  Salehe Banyanga. 


Akiongea na waandishi wa habari Alhaj Yusuph  Banyanga  amedai kuwa mnamo  tarehe  3 july alipigiwa simu na mtendaji kuhuhudhuria mkutano na wananchi wa eneo hilo ili kubaini chanzo cha  mgogoro uliopo. Lakin kwa mujibu wa  Alhaji Yusuph Banyanga  baada ya kufika eneo hilo la mkutano ambapo alikaribishwa na viongozi wa serikali , mwemyekiti, mtendaji pamoja na diwani ,  Yeye alijibu nanukuu" hata nishakaribia hata msingekaribisha". 

  Aidha  baada ya kauli hiyo alishambuliwa na yeye na familia yake..



Mtendaji wa kata hiyo amekiri kutokea kwa vurugu hizo baina ya familia ya Banyanga na wananchi,  na kusema kuwa wao kama viongozi  walijitaidi kuzuia vurugu hizo,  na kuwaahidi wananchi  kuleta wataalamu  wa ardhi ili kujiridhisha  uhakika wa mipaka na umilik halali wa eneo husika linaloleta mgogoro.


  Baadhi ya wananchi waliokuwepo eneo la tukio wamekiri kutokea kwa mgogoro huo na wamedai kua mwenyekiti wao mele sule ndie tatizo  .





Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI