Na junior Mwemezi Igunga Tabora
Wananchi mkoani tabora wameshiriki siku ya mkulima (Farmer Field Day) ambayo imefanyika katika kijiji cha Bwabakima kata ya Mbutu na Wilaya ya Igunga- Tabora
Mgeni rasim katika siku Mkuu wa Wilaya ya Igunga ambaye kutikana na majukumu mengine aliwakilishwa na Bi. Martha Teveli amewataka wakulima wa pamba katika wilaya ya Igunga kulima kilimo chenye tija na kufata ushauri wa wataalam wa kilimo kutoka Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania TARI
Siku hiyo imeudhuriwa na baadhi ya viongozi ambao ni pamoja mwakilishi wa ubalozi wa Brazil, Bodi ya pamba, mwakilishi wa Wizara ya Kilimo, wawakilishi wa uongozi wa Mkoa Tabora na wilaya Igunga, Wakulima hodari na Maafisa Ugani wa wilaya zote za Tabora, watafiti toka Makao Makuu Dodoma na TARI Ukiriguru -Mwanza.
Mradi wa Cotton Victoria ni matokeo ya ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Brazil katika kumsaidia mkulima kuzalisha zao la pamba kwa tija. Mradui huu ulianza mwaka 2017 kwa mikoa ya Mwanza, Geita, Simiyu, Shinyanga, Mara na sasa Tabora na Katavi.
Matokeo ya utafiti yamebainisha kuwa pamba ikipandwa kwa nafasi ya sentimita 60 kwa 30 (mbegu mbili kwa shimo) huwa na idadi ya
mimea 44,444 mara mbili ya aliyepanda kwa nafasi ya zamani ya sentimita 90 kwa 40 (mbegu mbili kwa shimo) ambayo huwa na idadi ya mimea 22,222 kwa eneo hilohilo.
Tija imeonekana kuwa kubwa kwa mkulima aliyepanda kwa nafasi ya sentimita 60 kwa 30 akifanikiwa kutunza vitumba 10 tu kwa kila mmea kwani ana uhakika wa kuvuna wastani wa kilo 700 hadi 1,400 kwa ekari (yasni kilo 2,000 hadi 3,000 kwa hekta) huku akiwa amefuata kanuni bora za kilimo cha pamba. Ukilinganisha na aliyepanda kwa sentimita 90 kwa 40 mavuno ni wastani wa kilo 200 hadi 300 kwa ekari.
Changamoto kubwa kwa wakulima wengi imeonekana ni kuchanganya pamba na nazao mengine na kutozingatia kanuni bora za kilimo cha pamba.
Hivyo, elimu ya upandaji kwa nafasi mpya na matumizi ya kanuni bora za kilimo cha pamba yamesisitizwa kwa wakulima hodari na maafisa ugani wa wilaya za mkoa wa Tabora walioshiriki mafunzo na Siku ya Mkulima kuwa mabalozi wazuri katika kusambaza teknolojia hii kwa wakulima wengine katika maeneo yao.










0 Comments