Header Ads Widget

DIWANI AJERUHIWA NA KWA KUPIGWA NA NONDO KICHWANI

 


NA HADIJA OMARY , MATUKIODAIMAAPP LINDI

Diwani wa kata ya Navanga halmashauri ya Mtama Mkoan Lindi Rashid Mkuya amejeruiwa kwa kupigwa na  kipande cha Nondo sehemu mbali mbali za mwiliwake na kusababisha majeraha kichwani na kifuani na watu wasio julikana 

Kwa mujibu wa Taarifa ya kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Lindi , Mtatiro Kitinkwi  inasema tukio hilo lilitokea jana  tarehe 12.06.2022 majira ya saa tisa usiku  huko kijiji cha Mkung'uni kata ya Navanga iliyopo Halmashauri ya Mtama Mkoani Lindi 

Tukio hilo limetokea wakati diwani huyo akijaribu kuokoa mali za mwananchi wake aitwaye AHMAD ALLY  aliyevunjiwa duka lake na kuibiwa pesa taslimu kiasi cha Tsh. 960,000/= ,TV moja FLAT aina ya EVOLLI nyeusi yenye thamani ya TSHS. 350,000/=

Hata hivyo taarifa hiyo inasema  TV hiyo alifanikiwa kuiokoa na majerhi amelazwa katika Hospitali ya MISSION NDANDA -Mkoani  MTWARA 

Aidha jeshi la Polisi Mkoani Lindi likishirikiana na wananchi wa vijiji jirani linaendelea kuwatafuta watuhumiwa hao. 


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI