Header Ads Widget

BILIONI 4 KUJENGA SHULE MAALUMU YA WASICHANA LINDI

 


NA HADIJA OMARY 



LINDI.....Katika kuboresha taaluma kwa watoto wa  kike  Mkoani Lindi , Serikali imetoa kiasi cha Shilingi milioni 4 kwa ajili ya ujenzi wa  shule maalumu ya Wasichana inayojengwa katika kata ya kilangala manispaa ya Lindi Mkoani humo



Katibu wa Itikadi na uenezi chama cha Mapinduzi CCM Shaka Hamidu Shaka leo mei 30 ameshiriki katika ujenzi wa shule hiyo katika kuunga jitihada za Serikali 




Akizungumza na wananchi Shaka aliwataka  wasimamizi wa Mradi huo kukamilisha kwa wakati ili uweze kuleta tija kwa jamii



Alisema lengo la Rais Samia kutoa fedha kwa ajili ya kujenga majengo ya kisasa na kuweka vifaa vinavyowavutia watoto kisaikolojia kupenda shule ni katika kuweka usawa kwa jinsia zote




Alisema kuwa ujenzi wa Shule hiyo ya wasichana ni miongoni mwa shule 10 zinazotarajiwa kujengwa hapa Nchini ambazo zimetengewa kiasi cha shilingi milioni tatu kila shule mmoja



Hata hivyo pamoja na mambo mengine Shaka aliwataka wazazi na walenzi Mkoani Huko kuhakikisha wanaungana kwa pamoja kupiga vita mambo yote yanayomdhalilisha Mtoto wa kike



Awali akitoa taarifa ya Mradi huo Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Lindi, Rehema Nahale alisema Ujenzi wa shule hiyo kubwa kuliko zote zilizopo Mkoa wa Lindi na Mtwara umeanza kutekelezwa mai 5 mwaka huu .



Shule hiyo  ya wasichana wenye vipaji na ufaulu wa kipekee  ni ya kidato cha kwanza na cha sita  ambapo mara tu itakapokamilika  itakuwa na uwezo wa kuchukua jumla ya wanafunzi 800.




Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bi Zainab Telack alisema Mkkoa huo wa Lindi kwa miaka mitatu mfululizo umekuwa ukiongoza katika Matokeo ya kidato cha sita , huku akieleza kwamba  ni mwaka jana tu imekuwa nafasi ya pili kitaifa hii ni baada ya shule moja kutoa watoto wanne kupata daraja la tatu.




Alisema Kutokana na usimamizi mkubwa unaofanywa na maafisa Elimu  na wakuu wa Shule wa  ufundishaji na usimamiaji wa Taaluma ndani ya Mkoa huo wa Lindi wanafunzi wengi watafaulu kwenda  kidato cha tano na wengi wao watabaki katika mkoa huo



Mwisho 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI