Na Hamida Ramadhan Matukio Daima APP Dodoma
MWENYEKITI wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki Adam Kimbisa amesema Baraza la Mawaziri wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zinatarajia kukutana kabla ya mwisho wa mwaka huu kutangaza kuongezeka kwa muda wa kuanza kutumika sarafu moja kwa nchi zote za Jumuiya.
Akiongea na waandishi wa habari leo April 6 jijini Dodoma Mwenyekiti huyo amesema Nchi zinazounda Jumuiya wanachama ni pamoja na Tanzania, Kenya,Uganda,Rwanda,Burudi,Sudani kusini na Kongo ambayo imemaliza mchakato wa kujiunga hivi karibuni
Amesema hatua ya kutumia sarafu moja ni muhimu katika kurahisisha biashara kwani itasaidia kuondokana na utaratibu wa kubadili fedha Kila unapovuka mpaka kwenda nchi nyingine.
"Majadiliano ya itifaki ya umoja wa fedha yalikamilika mwaka 2013 ambapo nchi wanachama zilikubaliana kuwa na kipindi Cha maandalizi Cha miaka 10 kuanzai mwaka 2014 na inatarajia kukamilika ifikapo 2024 na BARAZA la Mawaziri litakuta hivi karibuni kwà ajili ya kuongeza muda kwasababu bado mchakato haujafika kwenye hatua ambayo kufikia mwaka kesho kutwa itakuwa imekamilika,"amesema
Kimbisa amesema bunge la Afrika Mashariki limetunga sheria mbili za kuanzisha taasisi za Jumuiya zitakazosimamia mchakato wa umoja wa fedha na pia inaendelea na miswada mingine inayolenga kuanzisha taasisi zitakazosimamia utekelezaji wa umoja wa fedha.
Katika hatua nyingine Kimbisa amesema mtangamano wa afrika Mashariki ni katika shirikisho la kisasa ambapo hatua hiyo inalenga kuona Jumuiya ikiwa nchi moja yenye mfumo wa shirikisho ambao utasaidia kuongeza nguvu katika nyanja zote za kufanya kuwa wamoja zaidi.
Amesema katika kufikia hatua hiyo zipojuhudi zilizofanywa ikiwemo kuanzisha vyombo kama bunge la Afrika Mashariki, mahakama ya afrika Mashariki, mashirikiano katika masuala ya ulinzi na usalama na katika sera ya mambo nje.
Kwa mujibu wa Kimbisa amesema hatua ya umoja wa forodha ilianza rasmi mwaka 2005 baada ya nchi wanachama kuridhia itifaki ya umoja wa forodha na bunge la Afrika Mashariki ikatuka sheria ya kusimamia ambapo imesaidia kufungua milango ya biashara Kwa kuondoa ushuru wa forodha Kwa bidhaa zonazozalishwa ndani ya Jumuiya.
Ameeleza wananchi wanakuwa na uhuru wa kupeleka bidhaa zao katika nchi yoyote ambaye ni mwanachama bila vizuizi imesaidia kuongeza ukubwa wa Soko na ubora wa bidhaa kutokana na ushindani.
SOKO LA PAMOJA.
Kuhusu utekelezaji wa Soko la pamoja Kimbisa amesema mambo mbalimbali yamefanyika ambayo yameleta matokeo makubwa ya maendeleo ya Jumuiya ikiwemo uanzishwaji wa vituo 15 vya huduma za pamoja mipakani.
Ametaja juhudi nyingine kuwa ni utekelezaji wa himaya moja ya forodha, kuongezeka Kwa biashara ya ndani ya Jumuiya kutoka dola bilioni 1.6 Kwa mwaka 2005 hadi dola bilioni 3.2 mwaka 2020 na kuongezeka Kwa mitaji na Uwekezaji katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kimbisa amesema mafanikio yaliyopatikana kutokana na soko la pamoja ni kutolewa Kwa vitambulisho Kwa raia wa nchi wanachama, fursa za masomo , kufunguliwa Kwa fursa za ajira,baadhi ya nchi zimeondoa ada ya vibali vya kazi, kutolewa Kwa pasi moja ya kusafiria , kuondolewa Kwa vikwazo visivyo vya kiforodha, na kuanzishwa Kwa mamlaka ya ushindani Kwa nchi za Afrika Mashariki.
"Fursa zinahitaji watu wazichangamkie ili ziweze kuwaletea matunda watanzania tunapaswa kuzichangamkia fursa hizo Kwa kushindana na raia wa nchi nyingine wanachama ili tuweze kunufaika na mtangamano wetu na tafiti zinaonyesha kuwa moja ya vikwazo vinavyosababisha wanachama wengi washindwe kuzichangamkia fursa ni kutokuwa na uelewa wa kutosha,"amesema.
Kwa upande wake Mbunge Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki kutoka Zanzibar Maryam Ussy Yahya amesema katika Jumuiya hiyo wamependekeza jina la sarafu hiyo itakayotumika na nchi za umoja wa nchi za Afrika msahariki iitwe shilingi ya Afrika Mashariki.
Aidha amewataka watanzania kuendelea kuchangamkia fursa ya Soko la Afrika Mashariki ambapo hadi Sasa idadi imefikia watu milioni 270 hivyo ni uthibitisho tosha kuwa Kuna fursa za kutosha.
Tanzania inawakilishwa na Wabunge tisa katika bunge la Afrika Mashariki ambao ni Adam Kimbisa,Dkt Ngwaru Maghembe, Maryam Ussi Yahya,Dkt, Abdullah Hasnuu,Josephine Sebastian Lemoyan na Fancy Nkuhi.
0 Comments