Na Andrew Chale, Chalinze.
Mbunge Jimbo la Chalinze Mkoani Pwani na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Ridhiwani Kikwete amekagua ujenzi wa shule ya Sekondari inayojengwa katika Kijiji cha Msolwa huku akiwataka wazazi kuhimiza watoto wa kike kupatiwa elimu ilikuwa na akina Mama Samia wajao.
Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema hayo wakati wa leo Machi 7, wakati wa kukagua ujenzi wa shule ya Sekondari inayojengwa katika Kijiji hicho eneo la Makondo mengi
Ambapo amesema: "Mafanikio ya ujenzi wa Shule hii ya Sekondari Msolwa yanakwenda kuwezesha kuwapo kwa Wakinamama Samia wengi siku zijazo" alisema Mh. Kikwete
Na kuongeza kuwa, Serikali inafanya juhudi kuhakikisha wanasogeza huduma muhimu ikiwemo hiyo ya shule ambapo itakuwa mkombozi kutokana na watoto wanaofaulu kwenda mbali kufuata shule za sekondari.
"Tunashukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mh. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Shilingi Milioni 600 zilizowezesha ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Msolwa," Alisema.
Ujenzi wa shule hiyo utapunguza kero ya wanafunzi kufuata huduma hiyo mbali kwani wamekuwa wakipata changamoto mbalimbali wakiwemo watoto wa kike.
"Kazi Inaendelea Chalinze ili kuendana na kasi ya Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kutaka Kazi Iendelee" alimalizia Mhe. Ridhiwani.
Ujenzi huo naoendelea unatarajia kukamilika mwakani huku ikitarajiwa kuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi wa Msolwa na Vijiji jirani
0 Comments