Header Ads Widget

ULEGA AELEZA FURSA ZINAZOPATIKANA KWENYE UCHUMI WA BULUU


Serikali ya awamu ya Sita ya Mhe. Samia Suluhu Hassan kupitia programu ya kuendeleza kilimo na uvuvi (AFDP) imetenga takribani sh Bil 29 mwaka 2022/2023 kwa ajili ya kuwezesha kiuchumi shughuli za uvuvi na mikopo kwa wananchi waliopo kwenye sekta hiyo pamoja na kukuza pato la Taifa.


Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa mifugo na uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega wakati wa ufunguzi wa kikao  kazi cha mkakati na kampeni ya  kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe maji bahari kwa viongozi na  wataalam katika Mamlaka za Serikali za mitaa mkoani Tanga.



Alisema kuwa sehemu ya fedha hizo takribani sh Bil. 2.1 zinakwenda kukopeshwa kwa vikundi vya wafugaji wa samaki, wakulima wa mwani,wafugaji wa majongoo bahari,  wanenepeshaji wa kamba koche na  kaa, katika ukanda wa bahari ya Hindi.

 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI