Wananchi wa Kata ya Ruhembe Wilaya ya Kilosa Mkoa Morogoro wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia kiasi Cha shilingi Bilioni 1.2 kwa ajili ya ujenzi wa Daraja katika eneo hilo.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa eneo Hilo Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mheshimiwa Lazaro Londo amesema endapo Daraja Hilo litakamilika kwa wakati litainua uchumi wa wananchi wa Kata hiyo na Kata jirani .
Londo anasema watu kadhaa wamekufa maji wakati wakijaribu kuvuka mto huo hivyo wanamshukuru Rais Samia kwa fedha hizo alizowapatia
Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilosa Mhandisi Harold Sawaki anasema tayari wamemkabidhi mkandarasi aliyefahamika kwa jina la Kampuni ya Famost Company Ltd eneo la ujenzi wa Daraja kubwa la Ruhembe
Zawadi Anasema Daraja hilo litakua na ukubwa mita 40 na upana mita 9.84 na kinatarajia kukamilika kwa kipindi Cha miezi mitano
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Alhaj Majd Mwanga amemtaka mkandarasi huyo kukamilisha kwa wakati ujenzi wa Daraja Hilo
DC Mwanga anasema Rais Samia licha ya kutoa kiasi Cha shilingi Bilioni 1.2 ujenzi wa Daraja la Ruhembe lakini pia ametoa zaidi ya shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Berege wilayani humo
Shughuli hiyo pia imehudhuriwa na viongozi wa chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kilosa wakiongozwa na katibu wa ccm wilaya Shaban Mdoe ambapo amesema uujenziwa daraja Hilo ni utekelezaji wa ilani ya Chama Chama Cha Mapinduzi (CCM)
0 Comments