Header Ads Widget

MTUHUMIWA WA UJAMBAZI AJERUHI ASKARI KWA PANGA LILILOANDIKWA KIFO

  

ASKARI  polisi  watatu  Mkoani  Iringa,  wamejeruhiwa  sehemu  mbalimbali  za  miili  yao  wakati  wakimkamata   mtuhumiwa  sugu  wa  makosa  ya  wizi  wa  pikipiki   na  uvunjaji, Godson  Kahemela.

kamanda  wa  Polisi  Mkoa  wa  Iringa, Allan  Bukumbi` alisema  askari  hao  walijehuriwa  wakati  wakimthibiti  mtuhumiwa  huyo  ambaye   amekuwa  akijihusisha  na matukio   ya  uvunjaji  katika  maeneo  mbalimbali  manispaa ya iringa. mwandishi Francis Godwin anaripoti .

Kamanda   Bukumbi  alisema  ''Mtuhumiwa  huyu  wakati  anakamatwa   aliwajeruhi  askari  watatu   sehemu  mbalimbali   na  alipokamatwa  alikutwa  na  panga  aliloliandika  KIFO,   akimaanisha  kuwa  yuko  tayari   kufanya  mauaji   kama  ambavyo  alitaka  kuwafanyia  askari  wakati  anakamatwa,''  alisema  kamanda  Bukumbi.

Wakati  huo huo, Kamanda  Bukumbi   Jeshi  la polisi  kwa  kushirikiana  na  maofisa uhamiaji   wa  mkoa  wa  Iringa  wamewakamata  wahamiaji  40,  raia  wa  Ethiopia,  ambao  wanadaiwa  ya kuingia  nchini  kinyume  cha  utaratibu. 


Alisema  wahamiaji  hao  walikamatwa wilaya  Iringa  katika  Barabara  kuu ya  Iringa -Mbeya   baada  ya  kutelekezwa   katika   lori aina   ya  Mitsubishi   Fuso  lenye  namba  za  usajili  T 517 DJY  mali  ya  Deogratius  Kimambo,  mkazi  wa mkoani   Kirimanjaro.

Kamanda  Bukumbi  amesema  kukamatwa   kwa  wahamiaji hao  ni  muendelezo  wa  operesheni  mbalimbali  zinazoendelea  mkoani   Iringa   zenye  lengo  ya  kupambambana  na  matukio   ya  uhalifu.
Alisema  baada  ya  kufanya  upekuzi    katika  gari  hilo  walikutwa  wahamiaji  ha  wakiwa  wameingia  nchini  kupitia  mpaka  wa  Namanga, wakisafirishwa  kwenda  mpaka  wa Tunduma. 

Pia  alisema  Januari 11,  mwaka  huu  polisi  kwa  kushirikiana  na  maofisa  wa  hifadhi   ya  Taifa  Ruaha, waliwakamata  watu  wawili  wakisafirisha  meno  ya   tembo  vipande  19 pamoja  na  jino  moja  la  kiboko  kwa   kutumia  pikipiki 
Kamanda  Bukumbi aliwataja  watuhumiwa  hao  kuwa  ni  Ezekiel  Patrick (43) na  George  Ng'umbi  (25). Kadhalika,  alisema  januari  7,  mwaka  huu,  maeneo  ya  kitongoji  cha  Magunga  Bondeni,  Kiponzero  Wilayani  Iringa,  askari  polisi  walimkamata   Paul  Kalinga (47)  akiwa  na  meno  mawili  ya  tembo 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI