Header Ads Widget

"JAMII TUMIENI MAARIFA NA UJUZI KATIKA KULETA MAENDELEO"ASKOFU KIMARO

Askofu wa kanisa katoriki wa jimbo la Same,Rugath Kimaro amesema kanisa lina juhudi katika harakati za kuiwezesha jamii kwa kutumia maarifa na ujuzi katika kuleta maendeleo ya kweli.Mwandishi wa Matukio Daima Teddy Kilanga anaripoti toka Arusha 

Akizungumza katika chuo cha mtakatifu Agustine,Askofu Kimaro amesema lengo la chuo hicho kinalengo kuwa kituo bora cha elimu,utafiti pamoja na utumishi wa umma pamoja na kukuza harakati  na ulinzi wa kweli ulio katika uwazi na uaminifu na umahiri katika utoaji wa huduma

Askofu Rugath alisema pamoja na hayo pia chuo hicho kimelenga kutunza mali binafsi  na umma katika kuhamasisha maendeleo ya jumla katika utoaji wa elimu bora kwa uchambuzi na dhamira kwa kutoa huduma kwa ukarimu pamoja na heshima kwani ni tunu za masingi ambazo kama Taifa tunajivuania.

"Kanisa linatambua wazi kuwa ili kuwa na jamii yenye maendeleo ya kweli tunahitaji kufanya kazi kwa ushirikiano kwani tusipofanya hivyo twaweza kujenga matabaka yawaliyonacho na wasionacho,"amesema Askofu huyo.

Amesema wanapaswa kutumia rasilimali zilizopo ili kuiwezesha jamii  katika kuleta maendeleo ya kweli kama waliofanya watu mashuhuri duniani hivyo mabadiliko ya tabia ya nchi yanaleta madhara kwa jamii pamoja na kizazi kijacho.

Naye Mkurugenzi wa tawi la Arusha,Dkt.Charles Rufiriza amesema ni vyema jitihada za serikali zikazidi kubimarishwa ili watu wengi wapate kunufaika.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Mhandisi Richard Ruyango amesema anashukuru mamlaka za taasisi za dini kwa kazi  za utoaji wa elimu kwa watanzania kupitia taasisi zao za dini katika kutengeneza rasilimali za watu kwa kuleta maendeleo nchini.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI