Header Ads Widget

FAHAMU KUHUSU ISIMILA STONE AGE

  


Isimila ni eneo la kihistoria lililopo katika kijiji cha Ugwachanyakata ya Mseke, wilaya ya Iringa  mkoani Iringa  kusini mwa Tanzaniakilomita 20 kutoka Iringa mjini karibu na barabara kuu ya  Iringa – Mbeya

Njia ya kuingia si rahisi kuikuta: ukitokea Iringa iko kabla ya kufikia Tanangozi, upande wa kushoto,Eneo hili ni kivutio kimojawapo kinachoupamba mkoa wa Iringa.

Bonde la Isimila lilikaliwa na watu tangu Zama za Mawe za Kale  Ni katika eneo hilo ndipo zana za mawe za kale na nguzo za asili za Isimila zilipogunduliwa tangu mwaka 1951.

Zana hizo zinasadikiwa kuwa zilikuwepo tangu miaka 260,000 kabla ya Kristoumri uliopatikana kwa kupimwa mifupa ya kibinadamu iliyokutwa kati ya mawe yaliyochongwa kama zana

Miongoni mwa zana zilizopo katika korongo la Isimila, ambalo lina mikondo miwili, ni pamoja na mikuki iliyotumika kwa ajili ya kujihami na pia mawe ya kombeo kwa ajili ya uwindaji. Korongo la pembeni lina mmomonyoko wa ardhi ulioacha nguzo za ajabu.

Pia vifaa kama nyundo zilizokuwa zikitumika kwa ajili ya kutengenezea zana nyingine na shoka zilizotumika kwa kazi ya kuvunja mifupa, nyembe na visu.

Pia ndani ya eneo hili mafuvu na mifupa mingi vimeonekana; kati yake ilipatikana mifupa ambayo ilifanana na ya twiga wa hivi sasa, ila tofauti ni kwamba, mifupa hiyo iliashiria kuwa twiga hao walikuwa na shingo fupi, ambapo pia kulikuwa na aina tofauti ya viboko.

 

Kumbuka  utalii  ni moja kati ya  nguzo ya  uchumi wa Tanzania na  tayari  serikali imekuwa ikiwekeza  nguvu nyingi  zaidi katika kutangaza  utalii  japo kasi ya watanzania  kutembelea  vivutio  vya utalii  ni ndogo  sana  ukilinganisha na wageni  wanaofika katika  kutalii  kutoka nchi  mbali mbali  duniani .

 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI