Header Ads Widget

WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA

 


MAHAKAMA kuu  kanda ya  Iringa  iliyokaa kupitia  kikao chake katika mahakama  ya  hakimu mkazi Njombe ,imewahukumu  washtakiwa wawili   Manase Mhada (25) na Mwapulise Mfikwa (@()  kunyongwa  hadi kufa   baada ya  kukutwa na hatia ya  kumuua Eva Merikion Mgaya (28) nyumbani kwake  kijiji  cha Ihanga wilaya ya  Njombe.

Washtakiwa hao  walitekeleza  mauwaji hayo  baada ya  kumvamia nyumbani  kwake  Eva na baada ya   kufika kwa  lengo la  kuiba  mali.

Akisoma   hukumu  hiyo  jaji  Filmin Matogolo alisema  tukio   la mauwaji   lilitokea  may 8 mwaka 2015 baada ya wawili hao  kwenda  nyumbani kwa Wilfred Vitus Ng'olo  ambaye  ni  mume  wa  mareheme  wakiwa na bunduki  iliyotengenezwa   kienyeji  ambapo  walivamia na  kuiba  kwa  kunyang'anya  fedha  kwa  kutumia  silaha .

washtakiwa hao  pia  walichukua  simu ya mume wa  marehemu na  kumpiga  risasi Eva Merikion Mgaya  kifuani  kwa  kutumia bunduki  hiyo  na kusababisha  kifo  chake  papo hapo  kisha  kutoweka kabla ya  kukamatwa na baada ya  upelelezi wa  tukio hilo 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI