Header Ads Widget

WAHITIMU WA CHUO CHA CBE MWANZA WATAKIWA KUTOKATA TAMAA



Katibu Mkuu Wizara ya viwanda na biashara Dk  Dotto James amewasihi wahitimu  wa chuo cha CBE kutokata tamaa  ili kuweza kuyafikia malengo waliyojipangaia na kufanikiwa kimaisha. mwandishi wa matukio daima Chausiku Said anaripoti kutokea Mwanza

Wito huo ulitolewa katika mahafali ya 14 ya chuo hicho cha elimu ya biashara katika kampasi ya Mwanza na kueleza kuwa kufanikiwa ni lazima kuvaa uzalendo wenye heshima ili kupata taifa lenye maendeleo.

Dk James ameeleza kuwa ni vema wahitimu hao  kuwa na maadili mema ili kuweza kufikia malengo yao sanjari  na kuwa wabunifu  kwa kujishughulisha na shughuli mbalimbali kwa sababu ya uhaba wa ajira  ulipo nchini.

Ameeleza kuwa  kuna  taasisi nyingi za kifedha  ambazo zinakopesha pesa ni vema kuzitafuta ili kuweza kupata mikopo hiyo ili kufikia malengo ya kujikomboa na kuepuka kuwa tegemezi kwa familia na nchi  kwa ujumla

Aidha Dk james ameeleza kuwa chuo  hicho kina uwezo wa kudahili wanafunzi  2000 kutoka wanafunzi 400 hivyo  Serikali itaendelea kukitizama zaidi ili kuweza kumaliza changamoto ambazo wamezibainisha.

"Lengo la serikali ni kuona  chuo hiko kiendelea  kutoa elimu kwa wanafunzi ili waweze kupata elimu kama sera inavyotaka",amesema Dk James.

Naye Mkuu wa chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Emmanuel Mjema  amesema kuwa wanatarajia kuwaongezea  uwezo wahitimu  hao kwa kuwapa mipango ambayo itawasaidia wanafunzi  kuanzisha biashara zao  zitakazosaidia kujiajiri wenyewe.

"Tumeanzisha mpango mwingine wa mwanafunzi asome huku anafanya kazi tumeona wanafunzi wengi hawana ujuzi wa kufanya biashara kwani  kupitia mikakati hii tutawasaidia ili waweze  kujiajiri  na kuajiri watu wengine  kwani kufanya hivyo kutapelekea kunufaika na elimu wanayoipata kutoka  chuoni hapo.

Prof.Mjema aliongeza kuwa, chuo hicho kinatoa wanafunzi wenye weledi na watakaosaidia mambo mbalimbali katika jamii.

" Tunaishukru Serikali kwa  kutununulia eneo hili na majengo na sisi tutaendelea kufanya vizuri kwani viongozi mbalimbali wamesoma hapa ambao hivi sasa ni  Mawaziri, wafanya biashara wakubwa, hakuna kitakachoturudisha nyuma na kushindwa kuwasaidia na kuwapa ujuzi vijana hawa ili waweze kutimiza ndoto zao za baadae,"alisema prof Mjema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya uongozi wa chuo cha elimu ya Biashara Prof Wineasta Anderson alisema lengo kubwa la chuo ni kutoa wahitimu wanaojitambua katika tasinia mbalimbali ikiwemo ujasiliamali ili kutengeneza Taifa la watu wanaojitengemea ili  wakimaliza masomo yao waweze kujiajiri na kuajiri watu wengine.

Alisema wahitimu  hao watakuwa mabalozi wazuri kwa kujiari na siyo  kuwa tegemezi.

"Chuo hiki  kinakabiliwa na  changamoto mbalimbali tunaiomba Serikali iweze kututatulia zikiwemo za miundombinu ya barabara,umeme,na bweni la wanafunzi linahitaji kufanyiwa ukarabati,"alisema wineasta.

Jumla ya wahitimu 484 wametunukiwa Astashahada, Stashahada na Shahada wanaume 257 sawa  na  asilimia 53 na wanawake 227 sawa na asilimia 47 .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI