Header Ads Widget

RAS SENEDA; TUNAIPONGEZA SERIKALI CHINI YA RAIS SAMIA KWA KUTUPATIA FEDHA NYINGI ZA MAENDELEO MKOA WA IRINGA

 


SERIKALI ya  mkoa  wa  Iringa  imepongeza  jitihada  kubwa  zilizofanywa na serikali chini ya  rais Samia Suluhu Hassan kwa  kuupatia mkoa   huo fedha  kiasi cha  zaidi ya  shilingi  bilioni 8.6  wa  ajili ya  uteelezaji wa miradi ya mapambano dhidi ya UVIO -19.Mwandishi wa MDTV  Zacharia Nyamoga na Francis  Godwin  wanaripoti 

Katibu tawala mkoa wa Iringa  Happiness Seneda amesema  hayo  leo  wakati  akiwasilisha taarifa  ya utekelezaji  wa  miradi ya  kimaendeleo mkoa wa Iringa wakati wa kikao  maalum  cha madiwani wa halmashauri  zote za  mkoa wa Iringa  kilichofanyika Ukumbi wa Royal Pulm mjini Iringa .

Alisema  kuwa katika mwaka huu wa fedha 2021/2022 mkoa wa Iringa umepangiwa bajeti ya shilingi Bilioni 8,680,000,000.00 kwa ajili ya kutekeleza Mradi namba 5441 Mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19.

Aliongeza kwa kusema kuwa hadi kufikia mwezi novemba, 2021 jumla ya shilingi Bilioni saba milioni mia nane sitini na nane mia sita sitini na sita elfu mia tatu ishirini (7,868,666,320.00) zimekwisha pokelewa katikaHalmashauri.

Pia ametolea mchanuo wa pesa hiyo ambapo amesema shilingi bilioni sita milioni mia saba (6,700,000,000.00) ni kwa ajili uya sekta ya elimu, shilingi bilioni moja milioni mia moja ishirilini (1,120,000,000.00) ni kwa ajili ya sekta ya Afya na shilingi milioni arobaini na nane laki sita sitini na sita elfu mia tatu na ishirini (48,666,320.00) ni kwa ajili ya ufuatiliaji na tathimini ya miradi inayotekelezwa nchini ya mpango huu.

Sanjari na hayo  alizungumzia Changamoto za vifo vya kina Mama na kusema vifo vya kina mama vimezidi kuongezeka siku hadi siku Mkoani Iringa “Mlikuwa mnalalamika kuhusu kupigwa faini kwa wakina mama wanao jifungulia majumbani faini ile tumeitoa lakini tatizo linazidi kuongeka wakina mama hawafiki hospital wanajifungulia tu majumbani”  Amesema Seneda

Kwa kumalizia amewataka madiwani kuwasisitiza wananchi katika kata zao juu ya suala zima la Afya ilikujikinga na magonjwa mbalimbali yanayo samba na amewataka wanachini kuwa na tabia ya kujua Afya zao kwa kwenda hospital kujua Afya zao na kupata matibabu. 


Hata hivyo MNEC Salim Asas ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo ulio wakutanisha madiwani mkoa wa Iringa alipokuwa akizungumza amewaasa wakazi wa Iringa na Tanzania kwa ujumla kujikinga dhidi ya UVICO-19 kwa kufuata ushauri tunaopewa na wataalamu wa Afya ikiwa ni pamoja na kuvaa barakoa.


Mkutano umefungwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Dr  Nyamhanga huku akiwataka Madiwani kuyafanyia kazi yale waliyo afikiana kwa kuyaweka katika utekelezaji ili kuyafikia maendeleo amesema kama wasipo yafanyia kazi yale waliyo afikiana haita saidia kitu.

Kwa kumalizi haya pia  alisema wapo katika utaratibu kuhakikisha kuwa wana wainua wakina mama katika kuwapatia mikopo yenye tija na riba nafuu “Ifike mahala tuache kuwapa mikopo kama vipande vya nyama unakuta watu wapo 10 unawapa shilingi milioni moja yaani wagawane shilingi laki moja moja si kwelii jamani pesa hiyo itaishia katika kununua madela na vyombo tu na sikumuinua mwanamke” alisema  Dr  Nyamhanga
















Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI