Na Matukio daima media,Mbeya
MKUU wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Mbeya,Denis Manumbu ametoa onyo kali kwa watendaji na viongozi watakaobainika katika ufujaji wa fedha za Ugonjwa wa Uviko 19 ambazo zimetolewa na Serikali kwa ajili ya kufanya shughuli za maendeleo katika sekta ya Afya, Elimu na barabara.
Manumbu amesema hayo jana wakati akizungumza na Wanahabari ofisini kwake juu ya utekelezaji wa shughuli za Taasisi hiyo kwa kipindi cha robo ya mwaka kuanzia julai hadi septemba.
Aidha Manumbu aliema kuwa tayari Serikali imeingiza fedha za Uviko 19 kwenye Halmashauri zote za Mkoa wa Mbeya na kuwaomba watendaji na viongozi wote wa serikali wote watakaopewa nafasi ya kusimamia miradi kuwa waaminifu kujiepusha na vitendo vya rushwa.
“Nawatahadharisha watumishi wote wa umma fedha za Uviko 19 zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa kila Halmashauri imepewa fedha, tunaendelea kufuatilia na kufanya uchunguzi kwa yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria,” alisema Manumbu.
Hata hivyo Manumbu alisema kwamba kazi ya kuzuia na kupambana na rushwa itaendelea katika maeneo yote zikiwemo taasisi za umma na binafsi na kushauri namna bora ya kuiziba mianya hiyo.
"Natoa rai kwa wakurugenzi wa halmashauri zote za.mkoa wa mbeya kutoa ushirikiano wa hali ya juu wakati wa kutekeleza miradi ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya uvico 19 katika tawala za.mikoa na mamlaka za serikali za mitaa pindi utakapo hitajika"alisema Kamanda wa Takukuru.
0 Comments