Header Ads Widget

NAIBU WAZIRI MARY MASANJA ATOA UFAFANUZI KUHUSU USAFIRISHAJI WANYAMA PORI.

 



Na Hamida Ramadhan Dodoma 


NAIBU Waziri  wa Maliasili na Utalii Mary Masanja ametoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa za taharuki  zinazoendelea kusambaa katika ya mitandao ya kijamii  kwamba Serikali imaruhusu usafirishaji wa wanyama pori nje ya nchi.



Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini hapa  naibu waziri huyo amesema  mnamo tarehe 17 machi 2016  Serikali ilitoa tamko  la kuzuia  ukamataji na usafirishaji wa wanyamapori  hai nje ya nchi.


 Amesema kuwa , baada ya hatua hiyo, Serikali  iliamua kuwarejeshea wafanyabiashara  wa wanyampori  hai kiasi cha shilingi 173,289,430.60 ikiwa ni  nia ada mbalimbali walizolipa kabla ya kusitishwa kwa biashara hiyo.


Aidha , katika  ufumbuzi wa kudumu kufatia malalamiko  ya wafanyabiashara, Wizara  iliunda kamati ya waataalamu kwa ajili   ya kufanya  tathimini ya biashara ya kusafirisha  wanyamapori  hai nje ya nchi  na kuishauri Serikali kuhusu hatma ya biashara hiyo.


‘’  Baada ya tathimini ya kamati ya wataalamu , Wizara imeamua kufungua  biashara hiyo kwa kuruhusu usafirishaji wa wanyamapori  haikwa shaghuli za utafiti  wa kisanyasi na kidplomasia tu ,’’amesema Naibu waziri huyo.


Hata hivyo, amewataja wanyamapori hai ambao wanaruhusiwa katika usafirishaji  katika kipindi cha mpito  ni makundi  ya wadudu ( invertebrates) na wanyama pori jamii  ya ndege, reptilian, mammalia na amphibian, ambao jumla ni  aina 617 za wanyamapori  walioko kwenye mazizi.


Sambamba na hilo, amesema kwa sasa Serikali inaanda utaratibu  wa kuruhusu  biashara ya usafirishaji  kwa wanyama pori  waliokauushwa  na mazao ya wanyamapori  yaliyoongezwa thamani na itafanywa na wafanya biashara  wenye miradi  ya  ufugaji  wanyamapori  ili kuongeza  tija na kuhamasisha  ufugaji  wa wanyamapori.


‘’ Utaratibu  huu utakapoanza  kutumika  na kuwezesha  wafanyabiashara  wetu kuwekeza zaidi  kwenye  ufugaji  wa wanyamapori  pia  utasaidia kulinda kulinda sekta  ya utali kwa kuendelea  kuwavutia  wageni kuja nchini  kuona wanyamapori  hai wakiwa kwenye  mazingira yao ya asili’’ amesema.


MWISHO

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI