Header Ads Widget

MRADI WA RAFIC, DIT YAWANOA WAANDISHI NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI

 Na  Mwandishi Wetu. 

Taasisi ya Teknolojia Dar Es Salaam (DIT) Imefanya Semina ya Siku Moja na Waandishi Pamoja na Wahariri wa Vyombo vya Habari kuelekea kuanzishwa kwa  Kituo cha Umahiri wa  Teknolojia ya Habari na  Mawasiliano (Tehama),  kijulikanacho kama Regional Flagship ICT Center (RAFIC) ambapo Dola za Marekani milioni  16 zimewekezwa  katika Taasisi hiyo na Benki ya Dunia kwa lengo la kuendeleza ujuzi wa TEHAMA.



Akizungumza katika Semina hiyo, Mratibu wa mradi huo Dkt. Joseph Matiko aliongezea kuwa taasisi ya Teknolojia Dar Es Salaam kupitia Mradi huu inalenga  kutoa elimu ya kidijitali, kuongeza udahili pamoja kuwaandaa wanafunzi  waweze kujiajiri na kuajiriwa ndani na nje ya nchi.

“Kwenye huo mradi  wa RAFIC moja ya mambo  tunayolenga ni kutoa elimu  ya kidijitali ni mradi wa miaka  mitano na  umefadhiliwa na  Benki ya Dunia, ulianza  mwaka 2019 utamalizika  2024,” Mradi utainufaisha Taasisi kwa kiasi kikubwa mno ikiwemo kuboreka kwa mbinu za ufundishaji, ikiwemo kukamilika kwa ujenzi wa jengo kubwa la kisasa , kuwepo kwa vifaa vya ufundishaji pamoja na kuongeza ufahamu wa TEHAMA kwa walimu kwa lengo la kuendana na Teknolojia ya sasa. Alimalizia Dkt. Matiko



Kwa upande wake, Mwakilishi wa Wahariri na Waandishi wa Vyombo mbalimbali vya habari ameipongeza Taasisi ya Teknolojia Dar Es Salaam, kwa uamuzi wa kuamua kuanza na Waandishi katika utoaji wa Elimu juu ya Mradi huu, na kuahidi kuwa watakua bega kwa bega kuhakikisha wananchi wanahabarishwa kwa kina kuhusiana na mradi huu

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI