Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Said Ntahondi kwa niaba ya wenzake aliikabidhi barua hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani kwa ajili ya kumfikishia Rais Samia.
Alisema kwa kipindi kifupi cha uongozi wa Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia , Uyui imepata fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara.Alisema kati ya fedha hizo shilingi bilioni 2.4 ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya Sekondari na bilioni 1.1 kwa ajili ya vyumba vya madarasa katika Shule Shikizi.
Ntahondi alisema kuwa kiasi cha shilingi milioni 90 ni za ujenzi wa watumishi wa sekta ya afya na milioni 14.1 kwa ajili ya fedha za ufuatiliaji.
Alisema watahakikisha wanatumia kiasi cha milioni 20 kukamilisha darasa moja kama walivyoekelezwa na kiasi kingine kibaki .Ntahondi aliongeza hivi Madiwani na Watendaji wa Halmashauri hiyo wamejipanga kusimamia ili kuhakikisha fedha zinatumika kwa makusudio yaliyopangwa.
0 Comments