Header Ads Widget

SERIKALI YADHAMIRIA KILA MTANZANIA KUWA NA ANWANI YA MAKAZI

Serikali inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania imedhamiria kuhakikisha kwamba kila Mtanzania anakuwa

na anwani za makazi ifikapo mwaka 2022.

Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,

Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt.  Zainab Chaula katika semina ya kujenga

uelewa kwa Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania Bara kuhusu utekelezaji wa

mfumo wa anwani za makazi.

''Tunatarajia kufikisha mawasiliano mpaka vijijini, tunataka nchi nzima iwe na anwani

ya makazi'', amedokeza Dkt. Chaula.

Aidha, amehabarisha kuwa baadhi ya faida za kuwa na anwani za makazi ni

kurahisisha ukusanyaji kodi, kuwezesha biashara mtandao na kuimarisha ulinzi na

usalama.

Awali, akifungua semina hiyo, Katibu Mkuu wa  Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na

Serikali za Mitaa, Prof. Riziki Shemdoe amesema Serikali za Mikoa zina majukumu

ya kusimamia utekelezaji wa anwani za Makazi kwenye maeneo yao 

''Serikali yetu ya Tanzania kupitia Sera ya Posta ya mwaka 2003 imeimarisha

mifumo ya anwani za makazi inayoundwa na barabara, njia na namba za nyumba'', amebainisha.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya

Makazi, Mary Makondo amesisitiza ushirikiano ili kufikia malengo kwa kuwa moja ya

manufaa ya anwani hizo ni kuwezesha na kufanikisha utambuzi wa majengo na

viwanja vilivyopo ili kurahisisha kazi ya mipango miji na utekelezaji wa majukumu ya

kiuchumi na kijamii kwa Serikali na wananchi kwa ujumla

''Naamini tutaendelea kushirikiana katika kujenga nchi yetu na kuwahudumia

Watanzania'', ametanabaisha  Makondo

Ibara ya 61(m) ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020-2025

inaielekeza Serikali iliyopo madarakani kuhakikisha anuani za makazi zinawekwa

nchini ili kurahisisha upatikanaji, utoaji na ufikishishaji wa huduma mbali mbali kwa

wananchi.






Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI