Header Ads Widget

MAANDALIZI YA PAUL MWIJAGE CUP YAPAMBA MOTO, TIMU ZAANZA KUPOKEA VIFAA VYA MICHEZO

 



Na Mariam Kaagenda _Kagera 


Timu 20 za Mpira wa miguu  zinazotarajiwa kushiriki  Ligi ya Kamachumu Paul Mwijage Cup inayotarajiwa kuanza June 7 Mwaka huu zimepokea vifaa vya michezo pamoja na kanuni za mchezo huo .


Wakati akizungumza na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari Katibu wa Kamati ya maandalizi ya  Ligi  ya Kamachumu Paul Mwijage Cup 2026  Bwana Evodius Mariseli Angelo amesema kuwa lengo la Ligi hiyo ni kukuza na kutambua vipaji vinavyopatikana katika Tarafa ya Kamachumu wilaya ya  Muleba mkoani Kagera lakini pia na wananchi wa Tarafa hiyo kupata Burudani ya mchezo wa mpira wa miguu.



Amesema kuwa vifaa vilivyotolewa leo kwa timu zote 20 zinazotarajiwa kushiriki Ligi hiyo ni pamoja na mipira ili kuziwezesha timu hizo kufanya maandalizi mapema 


Ligi hiyo itazinduliwa rasmi June 7 Mwaka huu siku ya Jumapili ikiambatana na mchezo  wa Ngao ya Hisani  ambapo  Katibu huyo ameongeza kuwa Ligi hiyo itakuwa na Jumla ya Timu 20 na tayari Timu zote zimepata wachezaji na  zimeshakamilisha usajili na wamepata vibali vyote vinavyotakiwa.




Kwa upande wao baadhi ya Viongozi wa Timu zitakazoshiriki Ligi ya Kamachumu  Paul Mwijage Cup ambao ni Ally Raulenti kutoka timu ya Nyakahama FC, Eshibon Mganyizi timu Mafumbo A wamesema kuwa wamejiandaa vizuri kushiriki Ligi hiyo kwani wana wachezaji wenye uwezo mkubwa wa mchezo wa mpira wa miguu hivyo wameomba marefa wa mchezo huo kutenda haki pindi Ligi itakapoanza.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI