Header Ads Widget

TUWAKATAE WACHOCHEZI, GHASIA, VURUGU VINATURUDISHA NYUMA KIMAENDELEO



Mjasiriamali Kijana Bw. Peter Shaaban Gerald, Mkazi wa Kimara Dar Es Salaam amewasihi Vijana wenzake kujiepusha na uratibu na ufanyaji wa matukio ya ghasia na vurugu, yenye kuhatarisha amani ya Tanzania kwani athari za Kijamii na kiuchumi ni nyingi kutokana na mtindo wa maisha na namna ya kujipatia Kipato kwa Watanzania wengi hususan Vijana.

Ameyaeleza hayo wakati akizungumzia uzoefu alioupata kwa takribani siku saba zilizopita, zikitokana na uharibifu na ghasia za Oktoba 29, 2025 kwenye Majiji na Miji ya Dar Es Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya na Songwe, akisema uchumi wake umetetereka pakubwa kutokana na kukosa kipato kulingana na kazi yake ya kumtaka kuwa barabarani kila wakati ili kuwafuata na kuwatafuta wateja.

"Sisi tumezoea kutembea barabarani kujitafutia chochote, na unajua maisha ya Vijana ni gheto (Vyumba vya kuishi) sasa si sahihi kuandamana kwasababu sisi Vijana wengi tuliumia, wengine walizipoteza pia familia zao na tumezoea Tanzania ni nchi ya amani hivyo ni muhimu kuilinda amani yetu sisi kama Vijana." Amesisitiza Bw. Peter.

Peter amekumbusha pia wajibu wa Vijana katika kulinda amani ya Tanzania kwa msingi wa kuliandaa Taifa la kesho kutokana na nguvu kazi yao, akiishukuru serikali na Vyombo vya ulinzi na usalama kwa kurejesha amani katika maeneo yote nchini na hivyo kuruhusu shughuli za kiuchumi na kijamii kuweza kuendelea kama kawaida.



 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI