Header Ads Widget

‎DOTTO BAHEMU AWAHAMASISHA WANANCHI WA JIMBO LA NGARA KUJITOKEZA KUPIGA KURA ‎

 


‎Na Mariam Kaagenda _Kagera

‎Mgombea Ubunge wa  Jimbo la Ngara Dotto Jasson Bahemu  amewataka Wananchi  wa Jimbo hilo wenye sifa za kupiga kura kujitokeze kwa wingi  tarehe 29 Oktoba, 2025 kumchagua Rais, Mbunge na Madiwani .

Akizungumza na Wananchi katika mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Kata ya Bukiriro, mgombea huyo wa Ubunge ameomba kura za Mgombea Udiwani  kupitia Chama Cha Mapinduzi Bwana Erick Emily Nkilamachumu, kura za Mbunge Dotto Jasson Bahemu na Kura za mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan. 

Bahemu amesema kuwa zoezi la upigaji wa kura ni haki kwa kila Mtanzania mwenye sifa za kupiga kura hivyo  wananchi wa Jimbo la Ngara wanatakiwa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kupigia kura walivyojiandikishia ili kutimiza haki yao  

‎‎Akiomba kura za Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Bahemu amesema katika kipindi cha Miaka 4 Rais Samia amefanya mambo mengi ya maendeleo kupitia miradi iliyogharimu takribani kiasi cha shilingi  bilioni 81.

‎‎Aidha, amewataka Wananchi wote kuhakikisha wanapiga kura za ndiyo kwa wagombea wote wa Chama Cha Mapinduzi ili waweze kuharakisha maendeleo ya Jimbo hilo


‎‎


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI