Header Ads Widget

AMANI NDIYO UISLAMU, TUIHUBIRI NA KUILINDA- MUFTI ABUBAKAR

 

Na Matukio Daima Media

WAUMINI wa dini ya Kiislamu na Watanzania kwa ujumla wamehamasisha kujitokeza kwa wingi hapo Jumatano ya Oktoba 29, 2025 ili kupiga kura na kuwachagua Viongozi sahihi wanaoweza kuwaletea maendeleo sambamba na wote kuwajibika kuitunza amani ya Tanzania.

Wito huo umetolewa na Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir Ali Mbwawa wakati wa Mkutano maalumu wa viongozi na waumini wa dini ya Kiislamu Mkoani Njombe, Mkutano uliofanyika Masjid Taqwa, Mwembetongwa Mjini Makambako, akisema amani ndiyo nguzo muhimu ya maendeleo na ustawi wa Taifa, akiwataka waumini wa dini hiyo kuwa mfano wa kuigwa katika kudumisha utulivu na mshikamano.


"Niwakumbushe kuwa Mtume wetu ni mtume wa amani, ni Mtume wa Kheri, Mtume wa baraka na ameitangaza amani amani hiyo kama alivyoitangaza Mungu. Niwakumbushe Vijana amani ndiyo jambo kubwa kuliko yote asije mtu hapa akawadanganya kwaajili ya kuondosha amani halafu wewe ukakubali. Muislamu kila jambo ukiambiwa fikiria ujue linafaa au halifai lindeni amani Chungeni amani na kila mkipata hadhara simamemi semeni na hubirini kuhusu amani." Amesisitiza Mufti Abubakar.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI