Kikosi cha timu ya Mashujaa kilichotambulishwa katika Tamasha la timu hiyo lililofanyika mwishoni mwa wiki mjini Kigoma
Na Fadhili Abdallah,Kigoma
MKUU wa mkoa Kigoma Balozi Simon Sirro ametuma salam kwa timu za ligi ya Tanzania bara kuwa wasiichukulie poa timu ya Mashujaa kutoka mkoani Kigoma kwamba imejiandaa kuhakikisha inafanya vizuri katika ligi ya msimu huu.
Akizungumza katika tamasha la kutambulisha wachezaji wa timu hiyo maarufu kama Mashujaa Day Mkuu huyo wa mkoa Kigoma ametangaza dhamira ya ofisi yake kuiunga mkono timu hiyo sambamba na wananchi wote wa mkoa huo kuungana kwa hali na mali kuhakikisha malengo ya simu hiyo ya kufanya vizuri msimu huu kuelekea ubingwa yanafikiwa.
Mkuu wa mkoa Kigoma Balozi Simon Sirro akizungumza katika tamasha la Siku ya Mashujaa kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mjini




0 Comments