Header Ads Widget

QATAR YASEMA MSAKO UNAENDELEA KATIKA ENEO LA MASHAMBULIZI YA ISRAEL YANAYOLEGA VIONGOZI WA HAMAS

 

Mamlaka ya Qatar inasema bado inawasaka watu wawili waliotoweka na kuyatambua mabaki ya miili ya binadamu baada ya shambulio la Israel kuwalenga viongozi wakuu wa Hamas mjini Doha siku ya Jumanne.

Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kuwa kuna wasiwasi katika duru za kijeshi za Israel kwamba shambulio hilo lenye utata mkubwa halikufanikiwa.

Wizara ya mambo ya ndani ya Qatar imeitambua miili ya wanachama watatu kati ya watano wa ngazi ya chini wa Hamas ambao kundi lenye silaha la Palestina lilisema waliuawa pamoja na afisa wa usalama wa Qatar.

Hamas imedai jaribio la kuua timu yake ya mazungumzo lilishindikana. Katika mahojiano na CNN, waziri mkuu wa Qatar hakufichua hatma ya mpatanishi mkuu wa Hamas Khalil al-Hayya.

"Hadi sasa... hakuna tamko rasmi," Sheikh Mohammed bin Abdul Rahman Al Thani alisema Jumatano jioni.

Pia alisema hatua ya Israel ni sawa na "ugaidi wa serikali" na kwamba anatumai washirika wa likanda wa Qatar watakubali "jibu la pamoja".



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI