Header Ads Widget

KASULU KUANDAA BONANZA KUHAMASISHA MWENGE, UCHAGUZI MKUU


Na Fadhili Abdallah,Kigoma

Katika kuhamasisha ushiriki wa wananchi kwenye mbio  za Mwenge wa Uhuru September 17 na 18 na  Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka  huu   Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma imeandaa Bonanza  la Michezo litakalofanyika Jumamosi, Septemba 6 mwaka huu.


Mkuu wa wilaya Kasulu, Isack Mwakisu alisema hayo akizungumza katika kikao cha maandalizi ya Mwenge kilichokutanisha wadau kutoka sekta za umma na binafsi.


Mkuu huyo  wa Wilaya ya Kasulu  amesema bonanza kuwa hilo litakuwa chachu ya mshikamano wa wananchi kuelekea matukio hayo muhimu ya kitaifa.

Alisema kuwa Bonanza hilo  litafanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Kiganamo na litajumuisha michezo mbalimbali ambapo wito kwa  Wananchi wote kujitokeza kushiriki.

Mkuu huyo wa wilaya Kasulu alisema kuwa bonanza hilo litaanza kwa  matembezi ya pamoja kuzunguka mitaa  ya Kasulu mjini na baadaye  kurejea viwanja vya Kiganamo kwa michezo na shughuli za kijamii zitakazowaunganisha watu wa kada zote.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI