Na chausiku said
Matukio Daima Mwanza.
''Kama mtawapa motisha wakulima hatua hiyo itawasaidia kuongeza uzalishaji Bora na wenye tija na kupata kipato bora"Alisema Mtandao.
Kwa upande wake, Afisa Kilimo kutoka Bodi ya Pamba, Daniel Bariyanga, alisema halmashauri zote 54 zinazolima pamba zinapaswa kuhakikisha kila mkulima anayefanya vizuri anapewa zawadi.
Afisa Kilimo kutoka Bodi ya Pamba, Daniel Bariyanga akizungumza na waandishi wa habari akiwataka wakulima wa zao la pamba kuendelea kulipa Kwa tija
“Zawadi hizi zitakuwa kwa wakulima wanaozalisha kiwango kikubwa cha pamba kwa ekari. Wanaofanikisha kilo 1,000 au 2,000 kwa ekari watatunukiwa zawadi, ikiwemo mitungi ya gesi,” alisema Bariyanga
Aliongeza kuwa Bodi ya Pamba imejiandaa kusambaza pembejeo za kutosha kuanzia mbegu, viuatilifu, vinyunyizi na mbolea hai kwa wakulima wote ili kuongeza tija katika msimu ujao wa kilimo.
0 Comments