Mashambulizi mabaya ya Urusi katika mji wa Ukraine na miji mingine yaliendelea kushuhudiwa ikiwa imesalia masaa kadhaa kabla ya mkutano wa wa Volodymyr Zelensky na Donald Trump huko Washington.
Katika mji wa kaskazini mashariki mwa Kharkiv, watu wasiopungua wanne wakiwemo mtoto wamekufa wakati ndege isiyo na rubani ya Urusi iliposhambulia eneo la ghorofa, Meya wa jiji hilo Ihor Terekhov alisema.
Sehemu ya jengo imeanguka na watu zaidi inahofiwa wako chini ya vifusi.
Katika mkoa wa Zaporizhzhia, mtu mmoja alikufa na sita kujeruhiwa ikiwa ni pamoja na watoto wawili katika shambulio la Urusi kwa kutumia mabomu ya glide, mkuu wa utawala wa mkoa Ivan Fedorov amesema.
0 Comments